Meneja wa Masoko na Uhamasishaji wa Mfuko wa SELF- SELF MF, Linda Mshana kulia akimpa maelekezo Mkurugenzi Mkuu wa Star Natural Products LTD, George Buchafwe namna mfuko huo unavyotoa huduma zake kwa wananchi katika Maonyesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam na kushoto ni Meneja Mikopo Ufuatiliaji wa mfuko huo,Bw. Lucas Mlelwa.
Meneja wa Masoko na Uhamasishaji wa Mfuko wa SELF- SELF MF, Linda Mshana kulia na Meneja Mikopo Ufuatiliaji wa mfuko huo, Lucas Mlelwa kushoto wakitoa maelekezo kwa wananchi waliofika kujionea huduma zinazotolewa na mfuko huo katika Maonyesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. (Picha na Mpiga Picha wetu, Dar es Salaam).


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...