Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Plc kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji nchini wamezindua huduma mpya iitwayo ‘Malipo ya Pasipoti kwa M-Pesa’ katika hafla fupi iliyofanyika ofisi za makao makuu ya Uhamiaji, kurasini, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa M-Commerce, Epimack Mbeteni alisema huduma hii mpya inalenga kuwawezesha wateja wa kampuni hiyo kufanya malipo kwa haraka na urahisi zaidi. “Napenda kuwataarifu wateja wetu na Watanzania kwa ujumla kwamba, sasa wanaweza kulipia hati zao uhamiaji kwa kupitia M-Pesa”. 

“Ili mteja aweze kulipia inabidi aingie kwenye menu ya M-Pesa na kufuata utaratibu wa kulipa malipo ya serikali au kupitia zana (app) M-Pesa. Lengo letu ni kuhamasisha Watanzania wapate hati mpya za kieletroniki lakini pia kuwasogezea huduma za malipo viganjani kwao, ndio maana tumeona umuhimu wa kushirikiana na Uhamiaji kufanikisha hili” Aliongeza Mbeteni 

Huu ni mkakati wa kuwarahishia waombaji wa hati za kusafiria (Passport) ulipaji wa malipo kwa idara ya Uhamiaji, kwa vile walikuwa wakipanga foleni na kusubiria kwa muda mrefu ili kukamilisha malipo hayo 

Kamishna wa Passport wa Uhamiaji Marry Palmer alisema “tuna furaha kuungana na Vodacom Tanzania Plc kuwawezesha wateja kufanya malipo kirahisi, vile vile kuiwezesha idara yetu kufanya kazi kwa urahisi zaidi. Nategemea kuona bunifu nyingi zaidi kutoka Vodacom”. 

Vodacom imedhamiria kufikia idadi kubwa ya watu ambao hawapo kwenye mifumo rasmi ya kifedha, kuchochea ujumuishwaji, na uwezeshaji kupitia huduma rafiki na salama hivyo hii ni moja ya njia ya kufanikisha lengo hilo. 

“Tunaendeleza nia ya kubadili Tanzania kuwa jamii inayofanya malipo kidijitali, tunawekeza katika teknolojia ya simu ambayo itaingiza watu wengi zaidi katika mifumo ya kifedha na hatimaye, kufikia malengo ya kijamii na kiuchumi ya nchi”, alisisitiza mbeteni. 

Kampuni ya Vodacom imedhamiria kuipeleka Tanzania katika ulimwengu wa kidijitali ikiwa ni pamoja na kukuza matumizi ya pesa mtandao (E-money) kupitia mtandao wake ulioshamiri nchi nzima ambayo itasaidia wananchi kuepuka hatari mbalimbali zitokanazo na kubeba fedha kila wanapotaka kufanya manunuzi. 
Mkurugenzi wa M-Commerce Vodacom Tanzania, Epimarck Mbeteni akishikana mkono Kamishna wa Vibali, Mary Palmer, kuashiria uzinduzi wa huduma ya ‘Malipo ya Uhamiaji kwa M-Pesa’ wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi huo uliofanyika makao ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Wateja wa Vodacom sasa wanaweza kufanya malipo ya huduma za Uhamiaji moja kwa moja kupitia menu ya M-Pesa na Vodacom App.
Kamishna wa Vibali, Mary Palmer, (wa pili kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya ‘Malipo ya Uhamiaji kwa M-Pesa’ iliyofanyika makao ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Wateja wa Vodacom sasa wanaweza kufanya malipo ya huduma za Uhamiaji moja kwa moja kupitia menu ya M-Pesa na Vodacom App. Katikati ni Mkurugenzi wa M-Commerce, Epimarck Mbeteni, Mkurugenzi wa Wateja wa Mikataba (Business Enterprise Unit), Arjun Dhillon (wa pili kushoto) na Afisa Udhibiti wa Pasipoti, Peter Lucas Mwita (kushoto)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...