NA MWAMVUA MWINYI,CHALINZE
BAADHI ya watumishi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Chalinze, (CHALIWASA) wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wameaswa kuwa na lugha rafiki na nidhamu kwa wateja wanapokwenda kwenye ofisi badala ya kutoa majibu yasiyoridha hali inayosababisha malalamiko .
Kauli ya Mhandisi Raymond imefuatia malalamiko kutoka kwa Abdallah Kipolelo, aliyelalamikia kuwepo kwa baadhi ya viongozi wa CHALIWASA kutokuwa na lugha nzuri, mara baada ya kupokea taarifa za utendaji wa kazi kutoka kwa wateja.
Mkurugenzi Mtendaji wa CHALIWASA Mhandisi Honest Raymond, aliwaeleza watumishi watimize wajibu wa majukumu ya kazi na kufuata maadili ya kazi,wakati wa kikao cha kuwakumbusha majukumu yao kazini.
Kauli ya Mhandisi Raymond imefuatia malalamiko kutoka kwa Abdallah Kipolelo, aliyelalamikia kuwepo kwa baadhi ya viongozi wa CHALIWASA kutokuwa na lugha nzuri, mara baada ya kupokea taarifa za utendaji wa kazi kutoka kwa wateja.
“Sisi tunafundishwa namna ya kuwahudumia wateja, wao hawana somo kama hilo hivyo unapokutana na mteja anakuwa mkali, wewe jukumu lako ni kumtuliza, wakati mwingine anaweza kufikia hatua ya kukupiga ngumi inabidi mjue namna ya kuishi nao” alisema Mhandisi Raymond.
Kwa upande wake, Kipolelo alisem kuna wakati mtumishi anapokea simu ya upole kutoka kwa mteja akimjulisha kuwepo kwa uvujaji maji eneo alilopo, lakini utakuta kiongozi anajibu simu kwa ukali, hatua aliyodai kama ya udhalilishaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...