Katika kuunga mkono jitihada za serikali za kukuza sekta ya utalii nchini benki ya CRDB imezindua zao jipya la kibiashara liitwalo “SAFARI CAR LOAN”zao ambalo lina lengo la kuwawezesha  wajasiriamali waliopo katika sekta hiyo kufanya biashara yao kwa ufanisi kwa kuwapatia mikopo ya magari  mapya ya utalii kwa  riba nafuu 
Mkopo huo wenye riba ya asilimia 10 unatolewa na benki ya CRDB ambayo imeingia mkataba na kampuni ya utengenezaji magari maalum ya utalii ya Hanspaul ya jijini Arusha ambayo gari jipya hugharimu kiasi cha dola elfu sabini na tano hadi laki moja ambayo mkopaji atarejesha mkopo ndani ya miaka mitano.
Afisa  biashara Mkuu wa Benki ya CRDB ,Dakta Joseph Witts akizungumza hafla maalum ya uzinduzi wa zao hilo  la Safari Car Loan jijini Arusha iliyoenda sambamba na kongamano la utalii liloshirikisha a wafanyabiashara kutoka Hongkong China ,Tanzania na taasisi za serikali zinazojihusisha na uwekezaji dakta Witts alisema lengo la kuanzisha zao hilo ni kutatua changamoto ya usafiri usafiri katika sekta hiyo.
“CRDB tumekuja kutatua changamoto kubwa ambayo wafanyabiashara wamekuwa wakikumbana nayo kutokana na ukosefu wa mitaji ya kuweza kununua magari ya kusafirishia watalii tukijua kwamba utalii unachangia sehemu kubwa katika pato la taifa”alisema Witts.
Kwa upande wake Katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii profesa Adolf Mkenda aliipongeza benki ya  CRDB kwa uvumbuzi  wa zao jipya la kibenki ambalo litasaidia wajasiriamali kuweza kujipatia magari ya kusafirisha watalii kwa uhakika Zaidi.
“Uvumbuzi huu wa zao jipya la biashara la kibenk linasaidia wajasiriamali kuweza kujipatia magari ya kubeba watalii, huu ni ubunifu mzuri utasaidia vijana wetu ambao hawana mitaji mingi kuweza kujiingiza kwenye shughuli hizi hususani wakati huu ambao serikali ikiiendelea kuongeza vivutio vya utalii nchi”alisema Mkenda
Kwa pande wao baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo bi Fransisca Masika mkurugenzi wa  kampuni ya Nature Rensiposible Safari na S.M. Mwanonga mkurugenzi wa kampuni ya SAMLESS Adventures wameishukuru CRDB kwa mkopo huo ambao walisema utaboresha biashara yao.
 Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii profesa Adolf Mkenda (kulia) akipata maelezokatika halfa ya uzinduzi wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN unaotolewa na benki ya CRDB jijni Arusha. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa bodi ya utalii Tanzania jaji mstaafu Thomas  Mihayo 
 Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii profesa Adolf Mkenda (kulia) akikata utepe kuashiria  uzinduzi wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN unaotolewa na benki ya CRDB jijni Arusha
 Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii profesa Adolf Mkenda (kulia) akiwa katika moja ya gari katika halfa ya uzinduzi wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN unaotolewa na benki ya CRDB jijni Arusha
Moja ya gari katika halfa ya uzinduzi wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN unaotolewa na benki ya CRDB jijni Arusha
  Mwenyekiti wa bodi ya utalii Tanzania jaji mstaafu Thomas  Mihayo akimkabidhi ufunguo wa gari jipya mmoja wa wadau aliyenufaika na mkopo wa benk ya CRDB wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN uliozinduliwa jana jijini Arusha.
 Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii profesa Adolf Mkenda akimkabidhi ufunguo wa gari mkurugenzi wa kampuni ya utalii ya Samless adventures Sam Manonga baada ya kupata mkopo kutoka benki ya CRDB katika halfa ya uzinduzi wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN unaotolewa na benki ya CRDB.
 Mwenyekiti wa bodi ya utalii Tanzania jaji mstaafu Thomas  Mihayo akimkabidhi ufunguo wa gari jipya mkurugenzi wa kampuni ya Nature responsible safari  Bi Francisca Masika ambae ni mwanamke pekee aliyenufaika na mkopo wa benk ya CRDB wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN uliozinduliwa jana jijini Arusha.
 Mwenyekiti wa bodi ya utalii Tanzania jaji mstaafu Thomas  Mihayo akimkabidhi ufunguo wa gari jipya mkurugenzi wa kampuni ya Nature responsible safari  Bi Francisca Masika ambae ni mwanamke pekee aliyenufaika na mkopo wa benk ya CRDB wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN uliozinduliwa jana jijini Arusha.
 Katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii Profesa Adolf Mkenda akimkabidhi ufunguo wa gari jipya mkurugenzi wa kampuni ya Excelent guides Diason baada ya kupata mkopo wa  CRDB wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN uliozinduliwa jana jijini Arusha.
Katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii Profesa Adolf Mkenda akimkabidhi ufunguo wa gari jipya mkurugenzi wa kampuni ya Excelent guides Diason baada ya kupata mkopo wa  CRDB wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN uliozinduliwa jana jijini Arusha.

  Mmoja wa wadau akipongezwa kwa mkopo wa benk ya CRDB wa zao jipya la SAFARI CAR LOAN uliozinduliwa jana jijini Arusha.
 Wafanyakazi wa benk ya CRDB wakifurahia mapokeo ya  zao jipya la SAFARI CAR LOAN uliozinduliwa jana jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...