Na Catherine Sungura,WAMJW
Katibu Mkuu,Wizara ya Afya Dkt.Zainabu Chaula amewapongeza timu ya wizara ya afya , taasisi zake pamoja na manispaa ambao walishiriki kutoa huduma kwenye mkutano wa 39 wa SADC ulomalizika leo jijini Dar es Salaam.
Dkt.Chaula ametoa pongezi hizo baada ya kumalizika kwa mkutano huo na kukutana na timu hiyo na kufanya mazungumzo na watumishi hao."Mmefanya kazi kubwa na nzuri sana katika utoaji huduma kwenye mkutano huu hakika mnastahili pongezi".Alisema Dkt.Chaula.
Aidha, Katibu Mkuu huyo alisema kama mtendaji mkuu atatafuta namna ya kuwawezesha watoa huduma wengine kujengewa uwezo na timu hiyo mahali walipotoka ili kutembea pamoja katika kutekeleza mikakati ya sekta ya afya katika kuwahudumia wananchi wa Tanzania kwani wamepata ujuzi wa kutoa huduma hususani za dharura .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...