Jeshi la Polisi nchini limetoa ufafanuzi na kuweka
msisitizo kwenye katazo alilotoa Kamanda
wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam
tarehe 05/08/2019 kuhusu kupiga marufuku magari kufunga taa za vimulimuli au za
rangi rangi, taa zenye mwanga mkali (spot light) na kufunga ving’ora kwenye
magari ya kiraia au watu binafsi na pikipiki za kiraia.
Akitoa tamkoa hilo Msemaji wa Jeshi
hilo SACP David Misime amesema kuwa, katazo hilo ni kwa nchi nzima, kutokana na
kujitokeza kwa baadhi ya watu walioamua
kufunga vimulimuli na ving’ora na
kuvitumia wawapo barabarani na kusababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa
barabara. Wamefunga vifaa hivyo kutaka
kupewa kipaumbele wawapo barabarani kwa kujua au kwa kutofahamu kuwa ni
kinyume na sheria, kanuni na taratibu
zilizopo.
Na Kwa mujibu wa sheria ya
usalama barabarani sura ya 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka
2002 kifungu cha 39 B (I) na (2) kinafafanua juu ya matumizi ya ishara ikiwepo
ving’ora na vimulimuli.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...