Na Zainab Nyamka, Michuzi TV

WAWAKILISHI wa Michuano ya Kombe la Shirikisho CAF, Timu ya KMC imeweka wazi kikosi chake kitakachotumika kwa msimu wa mwaka 2019/20 kwenye Ligi kuu Tanzania Bara na Michuano ya kimataifa.

Kikosi hicho kitakachokuwa kinaongozwa na Kocha wa zamani wa klabu ya Simba Jackson Mayanja kina jumla ya wachezaji 28 kukiwa na usajili wa wachezaji wapya wa kimataifa.

Katika dirisha la usajili, Uongozi wa KMC uliweza kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji kwa kusajili mchezaji wa kitanzania aliyeongoza kwa magoli msimu uliopita Sali Aiyee, Vitalis Mayanga na kwa upande wa maeneo mengine waliweza kumsajili mchezaji wa zamani wa Simba Besala Bukungu na Jean Baptise Mugiraneza aliyecheza Azam.

Timu ya KMC itaanza kutupa karata yake ya kwanza kwenye michuano ya Kimataifa dhidi ya As Kigali Agosti 10 mwaka huu mechi itakayopigwa kwenye dimba la Kigali Stadium nchini Rwanda.

Wachezaji wengine ni Ismail Gambo, Serge Nogues, Cliff Buyoya, Denis Richard, Abdull Hilary, Charles Inlafia, na Ally Ramadhani, Amos Kadikilo, Ally Msengi,Juma Kaseja, Kelvin Kijili, Boniphace Maganga, Rayman Mgungila, Jonathan Nahimana, na James Msuva.

Wengine ni Sadala Lipangile, Kenny Ally, Yusuph Ndikumana, Abdallah Mfuko, Ramadhan Kapera, Hassan Kabunda, Mohamed Samata, George Sangija na Melly Sivirwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...