Mafundi wa DAWASA Mkoa wa Kawe wakiendelea na zoezi la ulazaji wa mabomba ya inchi 6 kwa umbali wa Kilomita 3 kutoka tanki la Changanyikeni lenye uwezo wa kuhifadhi lita 6,000,000, ili kuhudumia wakazi zaidi ya 500 wanaoishi katika kata ya Kibululu.

Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii
WANANCHI wa eneo la Kibululu Goba watafaidika na mradi wa maji wa Changanyikeni baada ya kukamilika kwa ulazaji wa mabomba.

Kazi ya ulazaji wa mabomba inaendelea chini ya mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam DAWASA.
Mafundi wa DAWASA Mkoa wa Kawe wameendelea kulaza mabomba ya inchi 6 kwa umbali wa Kilomita 3 kutoka tanki la Changanyikeni lenye uwezo wa kuhifadhi lita 6,000,000.

Kukamilika kwa mradi huo utawezesha kuhudumia wakazi zaidi ya 500 wanaoishi katika kata hiyo.

Wananchi wa kata ya Kibululu watafaidika na mradi huo mpyabaada ya kukaa kwa kipindi kirefu bila ya kupata maji safi na kwao ni neema na cherekoo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...