Na, Editha Edward-Tabora
Mwanamke mmoja mkazi Wa Goweko wilayani Uyui mkoani Tabora amemtahiri mtoto wake Wa kiume mwenye umri Wa mwaka mmoja na nusu kwa Kutumia Kisu kwa kile anachodai kuwa huwa anawatahiri watoto yeye mwenyewe bila kupata matatizo na huwa anafanya hivyo bila Kutumia ganzi
Kwa upande wao majirani zake walioshuhudia kitendo hicho walilazimika kumkamata na kumpeleka kituo cha polisi Goweko ambapo amechukuliwa yeye na mtoto wake na kukimbizwa hospitali Ili kwenda kuokoa maisha ya mtoto Huyo ambaye tayari Alikuwa amevuja damu nyingi hali iliyotishia usalama Wa mtoto
Akiwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa Wa Tabora kitete mtoto Huyo amepokelewa na kupatiwa huduma ya matibabu kwa haraka zaidi.
Pichani ni mama Wa mtoto aliyemtahiri mwanae Wa kiume kwa Kutumia Kisu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...