Kwa mara nyingine, mwimbaji wa nyimbo za Injili anayetikisa nchini Mariam Kilyenyi anatarajia kuachia albamu yake ya video inayoitwa Hakimu wa Haki katika uzinduzi utakaopambwa na waimbaji lukuki.
Uzinduzi huo unatarajia kufanyika Jumapili ya Septemba 29, 2019 kwanzia saa saba mchana katika kanisa la uamsho Pentecoste church kwa mchungaji Lilian Kadodo, Ubungo Shekilango.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mariam aliwataja baadhi ya waimbaji watakaomsindikiza kuwa ni DR Tumaini Msowoya Bahati Bukuku,Madame Ruth, Edson Mwasabwite Joyce Ombeni, Robert mwanja, Sarah Mghamba, Loyce Nducha Tumaini Njole, Stephania Masawe na Eddah Mwampagama.
Wengine ni Agnes Nkungwe, Elizabeth Shimanje,Jamuhury Zacharia, Tumaini Mwasubila, Hafsa kazinja,Magreth Sembuche Kisa ludutu Glory Moses ,Biver Kasigala, Surprise France silvia Alexander ,Neema Mahhu na Pst Grace Rendi
Aliwataja wengine kuwa ni w Dk Donald Kisanga, Stellah Joel,Alfonce Mutema, Daudi Nyigo, Yasinta Kadawele huku mwimbaji Jack Mgaza kutoka South Africa akiwa mmoja kati ya wageni maalum walioalikwa sambamba kabsaaaa na Agnese bilama kutokea Arusha.
Aliwataka wakazi wa Dar es Salaam na viunga vyake vyoooote kutokosa uzinduzi huo na kupata kazi yake mpya aliyofanikiwa kuiweka kwenye video.
Alitaja baadhi ya nyimbo zilizo kwenye albamu hiyo kuwa ni pamoja na Natafuta Mshauri, Agano Langu, Hakimu wa Haki, Pam Pam tukuza, Chereko leo, Ameshinda ,Laana imegeuka Baraka, Mapambazuko na Ushindi Lazima.
Mariam alisema japo ni gharama kubwa ya uandaaji wa muziki pamoja na kusambaza kazi hiyo lakini amefanikiwa kukamilisha albamu yake kwa mfumo wa video.
Mwimbaji wa Injili Mariam Kilyenyi pichani anatarajia kuzindua album yake ya Video hivi karibuni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...