Serikali ya mkoa wa Morogoro imetoa utaratibu kwa baadhi ya wadau
wa maendeleo watakao penda kuchangia msaada wa vifaa tiba kwaajili ya
majeruhi kupitia akauti ya bank ya NMB huku baadhi ya wadau hao wakiwemo
shirika la hifadhi za taifa tanapa wakitoa msaada wa kiasi cha shilingi
milioni kumi kwa ajili ya wathirika wa ajali ya lori lililolipuka kwa mato na kusababisha vifo zaidi ya 80 mpaka sasa.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk, Kebwe Steven Kebwe akipokea hundi ya
shillingi millioni 10 kutoka kwa Mhifadhi mkuu wa hifadhi milima ya Udzungwa, Donatus Dayona kwa niaba ya shirika la hifadhi za taifa TANAPA
kwa lengo la kusaidia waathiriwa wa ajali ya moto iliyotokea mkoani
Morogoro.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk,Kebwe Steven Kebwe akiwasikiliza kwa makini maofisa wa jeshi usu waliofika katika ofisi yake kwa mazungumuzo mbalimbali ikiwemo kutoa hundi ya shillingi milion 10 kwa ajiri ya kusaidia maafa yaliyotokea mkoani humo.
Mkuu wa mkoa wa morogoro Kushoto mwenye koti jeusi Dk,Kebwe Steven Kebwe akiongozana na maofisa wa jeshi usu mara baada ya kutoka kuona miili ya marehemu iliyokuwa nje ya chumba cha kuhifadhia maiti .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...