Serikali ya mkoa wa Morogoro imetoa utaratibu kwa baadhi ya wadau wa maendeleo watakao penda kuchangia msaada wa vifaa tiba kwaajili ya majeruhi kupitia akauti ya bank ya NMB huku baadhi ya wadau hao wakiwemo shirika la hifadhi za taifa tanapa wakitoa msaada wa kiasi cha shilingi milioni kumi kwa ajili ya wathirika wa ajali ya lori lililolipuka kwa mato na kusababisha vifo zaidi ya 80 mpaka sasa.
 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk, Kebwe Steven Kebwe akipokea hundi ya shillingi millioni 10 kutoka kwa Mhifadhi mkuu wa hifadhi  milima ya Udzungwa, Donatus Dayona kwa niaba ya  shirika la hifadhi  za taifa TANAPA  kwa lengo la kusaidia  waathiriwa wa ajali ya moto iliyotokea mkoani Morogoro.
 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk,Kebwe Steven Kebwe akiwasikiliza kwa makini maofisa wa jeshi usu waliofika katika ofisi yake kwa mazungumuzo   mbalimbali ikiwemo  kutoa  hundi ya shillingi milion 10 kwa ajiri ya kusaidia maafa yaliyotokea mkoani humo.
 Mkuu wa mkoa wa morogoro Kushoto mwenye koti jeusi  Dk,Kebwe Steven Kebwe  akiongozana na maofisa wa jeshi usu mara baada ya kutoka kuona miili  ya marehemu iliyokuwa  nje ya chumba cha kuhifadhia maiti .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...