Benki ya NMB imetoa msaada wenye thamani ya zaidi ya sh 50 milioni kwaajili ya kusaidia sekta za afya na elimu katika wilaya za Musoma na Butiama mkoani Mara. 

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo meneja wa NMB kanda ya ziwa Agustino Abraham alisema kuwa lengo la kutoa msaada huo nikutaka kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha huduma za kijamii hususan katika sekta ya elimu na afya. 

Alisema kuwa benki yake imeamua kusaidia sekta hizo hasa ikizingatiwa kuwa serikali ya awamu ya tano ina sera ya uchumi wa viwanda na kwamba sera hiyo haiwezi kufanikiwa endapo sekta za afya na elimu hazitakuwa imara. 

Alisema kuwa kutokana na umuhimu wa sekta hizo katika ukuaji wa uchumi wa taifa na jamii kwa ujumla benki yake imekwisha tumia zaidi ya sh 550 milioni kuboresha sekta hizo nchini kati ya sh 1 bilioni ambazo zimetengwa na NMB kwaajili ya kutoa msaada katika sekta hizo mwaka huu. 

Alisema kuwa msaada uliokabidhiwa ni pamoja na madawati , vitanda kwaajili ya wagonjwa na vingine kwaajili ya akinamama kujifungulia pamoja na mabati huku akisema kuwa msaada huo itanufaisha shule tatu za Msingi na tatu za sek9dari pamoja n.a. vituo vitatatu vya afya katika wilayani Musoma na Butiama.

Akipokea msaada huo, Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima aliishukuru benki hiyo ambapo alisema kuwa serikali imepanga kuboresha sekta za afya na elimu lakini juhudi hizi zinahitaji ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za kifedha. 

Malima alisema kuwa pamoja na kupokea msaada huo lakini serikali mkoani Mara bado inahitaji msaada na ushirikiano mkubwa kutoka kwa benki hiyo ili kuweza kuboresha mazingira ya elimu hususuan kwa watoto wa kike.

Alisema kuwa kutokana na mkoa wa Mara kuwa miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa vitendo vya ukatili , serikali mkoani humo imepanga kujenga makambi maalum maarufu kwa jina la nyumba salama kwa ajili ya kuwahifadhi watoto wa kike Ile waweze kuepukana na vitendo vya ukatili ambavyo kwa namna moja ama nyingine vimekuwa vikisababisha watoto wengi wa kike kuacha masomo na hivyo kushindwa kutimiza ndoto zao za elimu.

Malima pia ameitaka benki hiyo kusaidia katika kuboresha sekta ya kilimo kupitia mfumo wa NMB foundation kwa maelezo kuwa sekta ya kilimo ikiimarika ni dhahiri kuwa umasikini katika jamii utakuwa umetokomezwa na hivyo kufikia lengo la serikali la kuboresha maisha ya watanzania.

Akizungumza is niaba ya walimu walionufaika na msaada huo, Mkuu wa shule ya Sekondari ya Buhare iliyopo manispaa ya Musoma, Jonas Zakayo alishukuru NMB kwa msaada huo ambao alismea kuwa uatsaid8a katika kuboresha elimu na taaluma katika shule hizo.

Alisema kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na serikali katika kuboresha elimu lakini bado zipo changamoto mbalimbali ambazo zinatakiwa kutatuliwa kwa kushirikiana na wadau ili.elimu iweze kutolewa katika mazingira mazuri kwa manufaa ya kizazi kilichopo na kijacho.
Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima (wa pili kulia),Katibu Tawala wa mkoa huo Caroline Mthapula (kulia) wakipokea moja ya madawati zilizotolewa na NMB kutoka kwa Meneja wa Kanda ya Ziwa wa NMB Abraham Augustino (wa pili kushoto) na Meneja wa tawi la NMB Musoma Sebastian Kayaga (kushoto) , kwenye hafla iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Buhare. Benki hiyo imetoa msaada wa Sh 50Milioni ikijumuisha viti na meza 300 kwa ajili ya Shule sita, mabati 222 kwa ajili ya shule moja, vitanda vya kujifungulia, mashuka na vitanda vya kawaida vya hospitali kwa ajili ya vituo vya afya vitatu mkoani Mara.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Buhare, wakibeba viti baada ya kukabidhiwa na Benki ya NMB, katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika shuleni hapo. Benki hiyo imetoa msaada wa Sh50 milioni ikijumuisha viti na meza 300 kwa ajili ya Shule sita, mabati 222 kwa ajili ya shule moja, vitanda vya kujifungulia, mashuka na vitanda vya kawaida vya hospitali kwa ajili ya vituo vya afya vitatu vyote mkoani Mara
Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima (kulia) akipokea moja ya vitanda vya kawaida vya hospitali kutoka kwa Meneja wa Kanda ya Ziwa wa NMB Abraham Augustino, kwenye hafla iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Buhare. Benki hiyo imetoa msaada wa Sh 50Milioni ikijumuisha viti na meza 300 kwa ajili ya Shule sita, mabati 222 kwa ajili ya shule moja, vitanda vya kujifungulia, mashuka na vitanda vya kawaida vya hospitali kwa ajili ya vituo vya afya vitatu vyote mkoani Mara
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Buhare wakijisomea kipeperushi cha Benki ya NMB shuleni hapo wakati wa hafla ya kupokea msaada. Benki hiyo imetoa msaada wa Sh 50Milioni ikijumuisha viti na meza 300 kwa ajili ya Shule sita, mabati 222 kwa ajili ya shule moja, vitanda vya kujifungulia, mashuka na vitanda vya kawaida vya hospitali kwa ajili ya vituo vya afya vitatu vyote mkoani Mara 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...