Mwanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania kutoka Karatu Mkoani Arusha Bi Tarsila John akitoa maelekezo kwa mteja wake ya namna ya kutumia Mifuko y kuhifadhia Nafaka na Dawa za kuhifadhia nafaka, Bi Tarsila yuko katika maonyesho ya NaneNane kuelezea  ubora wa mifuko hiyo.
 Mwenyekiti wa Umoja wa wauza pembejeo wilayani kilombero mkoani morogoro ambaye pia ni mwanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania Bw John Bosco Zakaria Mvunjapori akitoa maelezo  kuhusu pembejeo za kilimo.
Mkazi wa Pawaga Mkaoni Iringa Bw. Twalibu Ubwa akifafanua jambo kwa wateja wake kuhusu bidhaa ya mchele, Ubwa ni mwanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania na yuko katika maonyesho hayo kuelezea namna wanavyoshiriki katika uongezaji thamani katika zao la Mpunga.
 Muonekano wa Banda la Baraza la Kilimo Tanzania katika Viwanja vya Mwl. Julias Nyerere Mkaoni Morogoro, ambapo Baraza limekuwa likishiriki kila mwaka maonyesho ya wakulima NaneNane, Fika katika banda lao ili uweze kupata taarifa sahihi kuhusu sekta ya Kilimo na mchango wake katika uchumi wanchi.

Bi Zaibab Mahenge kutoka Mafinga akiwa katika Banda la Baraza la Kilimo Tanzania akifafanua jambo kwa mteja wake aliyetaka kujua zaidi kuhusu bidhaa ya unga wa lishe inayozalishwa na Bi zainab ambayo inamchanganyo wa Unga wa Dona,Soya, Mbegu za Maboga, Ulezi na Mchele.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...