Mkuu wa kitengo cha Masoko na Uhusiano kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Bi. Theresia Mwami kulia akimpa maelezo kuhusu huduma za Wakala huo Meneja wa Tanesco mkoa wa Simiyu Mhandisi Rehema Mashinji wakati alipotembelea banda la TEMESA katika maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.
Afisa Uhusiano kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Bi. Beatrice Peter katikati akiwaelekeza watoto wa shule jinsi ya kuvuka barabara, kusoma alama za barabarani pamoja na jinsi taa za barabarani zinavyoongoza magari na watumiaji wake walipotembelea banda la Wakala huo katika maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.
Mohamed Mohamed kulia, dereva kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) akiwapa elimu kuhusu matumizi ya taa za barabara na alama zake baadhi ya washiriki wa Maonesho ya Wakulima Nanenane waliotembelea banda la TEMESA katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.
Fundi mwandamizi kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Luhende Matinde kushoto akiwaonyesha vijana wa shule jinsi ya kutambua vipuri feki na halali vya magari wakati walipotembelea banda la Wakala huo katika maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji TEMESA Hans Goodluck.

PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO (TEMESA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...