Timu ya wahadhiri na wanafunzi wa Chuo cha ustawi wa Jamii ikiongozwa na Mkuu wa taasisi hiyo Dkt. Joyce Nyoni wapo mkoani Morogoro kuanzia leo tarehe 13/08/2019 kuungana na timu ya maafa ya Mkoa wa Morogoro kutoa huduma za unasihi na huduma nyingine za awali za kisaikolojia kwa kuanzia na utambuzi wa mahitaji ya kisaikolojia ya wanafamilia hao.

Kwa kushirikiana na wataalamu wengine waliopo katika timu hiyo, Chuo cha Ustawi wa Jamii kitashiriki katika kupanga huduma na utekelezaji wa mpango wa huduma kwa familia hizo.

Katika kufanikisha zoezi hili timu ya maafisa ustawi inafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu sana na serikali za mitaa kuhakikisha kila kaya iliyofikwa na msiba au kupata majeruhi ya ajali hii mbaya ya moto zinatambuliwa mahitaji yao ya kisaikolojia na kupata huduma stahiki.
Mhadhiri msaidizi wa Chuo cha ustawi wa Jamii Abigail Kiwelu kutoka idara ya taaluma ya ustawi wa jamii na Afisa ustawi wa Jamii Subisya Kabuje kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi (wenye makaratasi) wakizungumza na mama mzazi (wa kwanza kushoto) na dada (wa pili kushoto) wa mmoja wa wahanga aliyepoteza maisha kwenye ajali ya moto msamvu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...