Na Woinde Shizza Michuzi Tv ,Arusha.

Imebainika kuwa wakulima wengi hapa nchini hawana taaluma ya kutosha ya kanuni za teknolojia ya unyunyiziaji wa viuatilifu hali inayopelekea viuatilifu hivyo kutofanya Kazi jinsi inavyotakiwa ,kitu kinachofanya wakulima hao kulalamikia viuatilifu hivyo nivibofu na havifanyi kazi 

Hayo yamebainishwa leo na Mkuu wa kitengo cha unyunyuziaji wa viuatilifu vya kuulia wadudu kutoka TPRI Julius Mkenda wakati akiongea na waandishi wa habari ndani ya maonesho ya nane nane yanayofanyika katika viwanja vya nane nane vilivyopo Themi njiro jijini hapa, ambayo kwa mikoa ya Kanda ya kaskazini yanafanyika mkoani hapa.

Alibainisha kuwa wamepokea malalamiko mengi kutoka kwa wakulima kuwa viuatilifu hivyo vya kuulia wadudu havifanyi Kazi na walipofanya uchunguzi waligundua kuwa tatizo halipo katika viatilifu Bali tatizo lipo kwa wakulima kwani hawana Elimu ya kutosha ya namna yakunyunyuzia viuatilifu hivyo.

"Tumepata malalamiko sehemu nyingi ikiwemo kwenye Korosho ,Pamba ,mbogamboga na maeneo mengine mengi ambayo tumekuwa tukiusika na wakulima na katika Utafiti tuliofanya na ufatiliaji tulioufanya tuligundua kuwa tatizo kubwa la wakulima ni kutonyunyiza viuatilifu kwanamna ambayo inavyotakiwa " alisema Mkenda

Alibainisha kuwa kutokana na kugundua tatizo hilo wao kama TPRI wameamua kuzunguka nchi nzima na kutoka mafunzo kwa wataalamu wa Kilimo ,maafisa Kilimo,wafanyabiadhara wa viuatilifu na wasambazaji wa viuatilifu pamoja na wakulima na pia wamewajengea uwezo wa ufahamu wa kanuni sahihi za unyunyuziaji wa viuatilifu ,pamoja na kuwafundisha kanuni na ufahamu wa uelewa wa matumizi sahihi ya vinyunyizi vinavyotumika katika kunyunyiza viuatilifu .

"Kuna vivyunyizi na vinyunyizo kwa hivyo wakulima wengi hawajui matumizi vinyunyizi yaani vile vitundu na tumekuwa tukiwafundisha kwasababu ,kinyunyunyizo hiki ndicho kinachotengeneza aina ya matone yanayo muangamiza kisumbufu yaani mdudu na kila mdudu ana aina ya matone yanayo muangamiza ,na tunatoa hii taaluma ili kuweza kuhakikisha wakulima wanafanikiwa kuwaangamiza hawa wadudu visumbufu" alibainisha Mkenda 

Kwa upande wake mtafiti mwandamizi wa visumbufu na viuatilifu Maneno Chidege alisema kuwa kwa sasa hivi kuna aina tatu ya vishambulizi ambayo vinasumbua sana wakulima ,kimoja wapo ya vishambulizi na visumbufu hicho ni viwavijeshi vya maize ambayo viliingia hapa nchini mwaka 2017 na huyu mdudu akuwepo hapa nchini naali sema mdudu huyu amevamia nchi huyu ni mdudu vamizi ,pia kuna mungine anaitwa kantangaze huyu akiwa anashambulia nyanya sana wote hawa wameingia hapa nchini kwani awali hawakuwepo ,na hadi sasa wamefanya Utafiti na wamegundua dawa , namna ya kuwathibiti wadudu hawa ambapo alibainisha kuwa njia pekee ya kuwaangamiza wadudu hawa ni pamoja na kuzingatia kanuni za mafunzo wanazopewa,pamoja na kuachana na tabia ya mazoea pia watumie taaluma mpya wanayopewa kwani watapata mafanikio

Aidha aliwataka wakulima kutopiga dawa holela bila kupata ushauri wa bwana shamba au wao wenyewe watafiti maana wanapopiga dawa holela kwanza wanamtengenezea mdudu usugu ,pili watakuwa wanamaliza fedha zao bure bila kupata mafanikio wala manufaa yoyote, pia inaweza isishambulie,pia utakuwa umeumiza mazingira ya kwenye udongo maana kila mdudu ana sumu ambayo inamzibiti.
Mkuu wa kitengo cha unyunyuziaji wa viuatilifu vya kuulia wadudu kutoka TPRI Julius Mkenda akitoa maelekezo kwa wakulima waliotembelea banda LA TPRI hawapo pichani kupata Elimu. 
Mtafiti mwandamizi wa visumbufu na viuatilifu Maneno Chidege akielezea aina za wadudu wanaosumbua wakulima 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...