Imani Sichalwe Kaimu Msajili wa Bodi ya nyama Tanzania akizungumza katika Maonyesho ya Teknolojia za Uchakataji wa nyama Jijini Arusha.
Na.Vero Ignatus Arusha.
Bodi ya Nyama nchini imepiga marufuku matumizi ya magari yenye kutu katika kubeba nyama kwani kutu ni hatari kwa afya ya binadamu hivyo amesema kuwa serikali haitasita kuchukua hatua kali kwa watakaokahidi agizo hilo.
Imani Sichalwe ni Kaimu Msajili wa Bodi ya nyama Tanzania akizungumza katika Maonyesho ya Teknolojia za Uchakataji wa nyama yaliyohudhuriwa na Wanachama wa Chama cha Wachinjaji na Wafanyabiashara wa nyama jijini Arusha ,amesema wamechukua hatua hiyo ili kulinda ubora wa nyama na kulinda afya za walaji kwa kihakikisha magari yenye kutu hayataruhusiwa kubeba nyama pamoja na ubebaji wa nyama mgongoni.
Alex Lasiki ni Mwenyekiti wa Chama cha Wachinjaji ameiomba serikali isogeze mbele katazo hilo la kutumia vigogo vya miti kukata nyama na kuweka mashine za kukata nyama kwani wachinjaji wengi wanakabiliwa na changamoto ya mitaji midogo ili waweze kujipanga kununua mashine za kisasa.
Ismail Kulanga ni Mkurugenzi wa Jiji la Arusha amesema kuwa jiji la Arusha litashirikiana na machinjio ya Arusha Meat ili kuboresha mazingira ya machinjio hayo na kuhakikisha huduma bora zinatolewa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...