Famasi ya dawa iliyoko kwenye hospitali ya rufaa ya kanda ya bugando iliyoko

Jengo la huduma za dharura na ajali ambalo linatoa huduma zote zikiwemo za upasuaji

******************

Na.Catherine Sungura-Mwanza

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando(BMC) ipo mbioni kuanzisha taasisi ya moyo ili kuweza kuhudumia wananchi wa kanda ya ziwa.

Akiongea kwenye mkutano wa maofisa habari wa wizara na taasisi wake pamoja na waandishi wa habari jijini hapa mwishoni mwa wiki,Mkurugenzi wa hospitali hiyo Prof. Abel Makubi alisema kuwa wapo mbioni kuanzisha taasisi hiyo itakayokuwa na majengo mawili yenye ghorofa kumi na kumi na tano.

Prof. Makubi alisema kuwa hadi kukamilika kwa majengo hayo wanatarajia kutumia shilingi bilioni 59 .

“Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kwa dhati kutoa huduma zote za kibingwa na bobezi hapa nchini,hii itapunguzia mzigo serikali na wizara kupeleka wagonjwa nje ya nchi vilevile wananchi wa kanda hii kunufaika na huduma za moyo huku huku”.

Kwa upande wa watumishi Prof. Makubi alisema wameweza kuongeza wataalam wa fani mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wakiwepo wauguzi,madaktari,madaktari bingwa na bobezi na hivyo kufanya kazi ya utoaji huduma katika idara zote bila kuteleleka.

Hata hivyo ameishukuru serikali ya Tanzania kwa kusomesha madaktari bingwa na bobezi kutoka hospitali hiyo na hivyo kuifanya hospitali hiyo kutoa huduma za kibingwa ikiwemo matatizo ya tumbo,mifupa,koo,pua na ndomo,macho,mfumo wa mkojo,meno,ubongo na mishipa ya fahamu pamoja na matatizo ya akina mama.

“Huduma za upasuaji kiujumla zimeboreka sana katika awamu hii kwa upande wa upasuaji mkubwa wa kawaida pia,upasuaji maalumu wa midomo sungura,kichwa maji na mgongo wazi pamoja na upasuaji wa fistula”.Aliongeza Prof. Makubi

Aidha,aliishukuru Hospitali ya Taifa Muhimbili na Taasisi ya Mifupa MOI kwa,mashirikiano ya karibu katika kutoa huduma za kibingwa,za upasuaji katika mikoa mbalimbali ya kanda ya ziwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...