Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe Patrobas Katambi akiwa na viongozi wa Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo sambamba na watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo.

Charles James, Michuzi TV

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe Patrobas Katambi amemshukuru Rais Dk John Magufuli kwa namna alivyotekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi ndani ya kipindi kifupi. 

DC Katambi amesema Rais Magufuli amefanya mambo makubwa kwenye afya, elimu, miundombinu na miraidi ya maendeleo na kuwataka Watanzania kuzidi kumuombea.

Amesema zawadi pekee ambayo imekua Watanzania wanaweza kumpatia Rais Magufuli kutokana na utendaji kazi wake basi ni kufanya kazi kwa bidii, kuwa wazalendo na kuweka maslahi ya Taifa mbele.

" Hakuna Taifa lolote duniani ambalo limefanikiwa bila kufanya kazi siri yao kubwa kuwa na umoja wa kitaifa, mshikamano na upendo hivyo ni vema Watanzania tukawa na upendo na Serikali yetu hii ambayo inafanya kazi usiku na mchana kutuletea maendeleo.

" Lakini jambo lingine na kubwa la kumpatia Rais Magufuli ni kumwaga kura nyingi sana mwakani kwenye uchaguzi Mkuu kwa sababu kwa haya mambo makubwa anayofanya Reli ya Kisasa, Bwawa ka Umeme, Ndege, Ubanaji wa matumizi na kuzuia ufisadi vyote hivyo vinatosha kumfanya asiangaike kuomba kura," Amesema DC Katambi.

Akizungumza mbele ya kamati ya siasa ya Wilaya hiyo, DC Katambi amewaahidi kuendelea kusimamia kwa upana maslahi ya umma na mtumishi yeyote atakwenda kinyume na maagizo na kasi ya Rais Magufuli hatosita kumchukulia hatua.

Amesema kwenye maeneo ya kuchukua hatua ataendelea kuchukua hatua bila kumuonea mtu.

" Lazima tugombane tunavyoona mtu hafati misingi ya utumishi ya umma na niwaambie watendaji na watumishi wote waliopo ndani ya Wilaya hii sitomchekea mtu hakuna udugu wala urafiki kwenye mali za umma. Kwa viongozi wenye kasoro mimi sina unafiki. Kabla sijatumbuliwa mimi mwingine atakua amesagwa kabisa," Amesema DC Katambi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...