***************

Jeshi la Polisi kupitia kikosi chake cha Reli leo kimetoa Elimu kwa Abiria
wanaotumia usafiri wa Treni juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na uhalifu
unaofanywa na baadhi wa matapeli, elimu hiyo imetolewa na SGT Michael,
eneo la kamata kariakoo jijini Dar Es Salaam mapema leo kabla abiria hao
kuanza safari ya kuelekea Mkoani Kigoma. Huku akisema kwa kipindi kifupi
ambacho safiri za treni zilisimama baadhi ya watu walitumia nafasi hiyo kamasehemu ya kujipatia kipato kwa kuwatapeli abiria kwa njia ya kukatisha tiketifeki.

Aidha katika hatua nyingine SGT Michael aliwataka wanandoa pamoja na
watu wengine wanaotumia usafiri huo kuacha kuwafanyia ukatili wa kijinsiawenza wao au watoto wao huku akisema kuna baadhi watu husafirisha familiazao hasa kwa wanawake wajawazito ambao wamekaribia kujifungua hali hiyohuwapelekea wanawake hao kujifungulia ndani ya Treni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...