Kamati ya Usalama Barabarani mkoa wa Morogoro wamekutana na nakufanya mazungumzo na Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Shaka Hamdu Shaka ofisini kwake.
Kamati hiyo ikiongozwa Mwenyekiti wake Ndugu Johanes Kakiziba pamoja na mambo mengine waliwasisha mpango mkakati wao wa utekelezaji wao katika kipindi cha miezi sita ijayo.
“Sisi tuna makundi ya mjumuiko wa watu katika jamii, ili muweze kufanikisha majukumu wenu lazima sisi tuwe mabalozi wenu wazuri kwa vile mara nyingi hukutana nao katika shuhuli mbali mbali, vyengine kazi yenu itakuwa ngumu”
“Naelekewa zipo changamoto za usalama barabarani katika mkoa wetu Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Morogoro tuko pamoja na nanyi”
“Endeleeni nasi tutawaunga mkono ushauri wangu kwenu mipango yenu isishie kwenye makaratasi lazima mjipange vizuri katika usimamizi na utekelezaji wake, punguzeni urasimu wa kuwa mbioni kukamilika kila siku hatamfanikiwa na mwisho wa siku mtaonekana nanyi ni mizigo isiyobebeka mbele ya mamlaka hata wananchi” Shaka Hamdu Shaka.
Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...