Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Kukamilika kwa mradi wa Kisarawe kutanufausha mji mzima wa kisarawe, eneo la sekta viwanda na vitongoji jirani na mji huo.

Tatizo la Maji kwa Wananchi wa Kisarawe litabaki historia baada ya mradi wa ujenzi wa Tanki la maji lenye ujazo wa lita Milion sita kukamilika.

Mradi huo uliozinduliwa na Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu utawanufaisha wananchu wa eneo la Kisarawe na maeneo ya Viwanda.

Ujenzi wa Mradi huo unasimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) ambao umechukua takribani miezi 12 kukamilika.

Akitoa taarifa ya kukamilika kwa mradi huo ambao kwa sasa mkandarasi anaendelea na kazi ya uunganishaji wa bomba, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Jamii DAWASA, Neli Msuya amesema kwa sasa Mkandarasi sambamba na mafundi kutoka Mamlaka hiyo wanaendelea na maunganisho ya bomba la nchi 16 kutoka Mtambo wa Ruvu juu kuelekea kwenye tanki la Kisarawe.

Amesema, maunganisho ya bom a hilo yanafanyika kwenye mradi wa Kibamba ambapo mafundi wapo katika hatua za mwisho kukamilisha.

Wakazi wa Kisarawe watanufaika na mradi huo ambapo wamekuwa na kero ya maji kwa muda mrefu na kukamilika kwake kutatatua changamoto hiyo pamoja na kuvutia wawekezaji kwenda kuwekeza kwenye maeneo ya viwanda.

Mradi wa Kisarawe unajengwa kwa fedha za ndani za Mamlaka ya Majisafi na Majitaka DAWASA na unagharimu takribani Bilioni 10 za kitanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...