Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Kaimu Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa Tanzania Ettienne Ndayiragije ameita kikosi cha Wachezaji 25 kwa ajili ya kujiandaa na mchezo dhidi ya Sudan.

Kikosi hichi kinatarajia kuingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na mchezo huo wa Kufuza CHAN mwaka

Wachezaji walioitwa ni Golikipa Juma Kaseja (KMC),Metacha Mnata (Yanga) na Said Kipao (Kagera Sugar).  Kwa upande wa safu ha ulinzi ni Haruna Shamte (Simba), Gadiel Michael (Simba), Mohamed Hussein (Simba), Kelvin Yondani (Yanga) Boniface Maganga (KMC) na Erasto Nyoni (Simba).

Wachezaji wengine, ni Iddy Mobi (Polisi Tanzania), Bakari Nondo (Coastal Union), Jonas Mkude (Simba),  Bakari Majogori (Polisi Tanzania), Mohamed Issa (Yanga), Iddy Selemani (Azam), Mudathir Yahya (Azam) na Salum Abubakar (Azam)

Wengine ni Frank Domayo (Azam), Mzamiru Yassin (Simba),  Shaban Idd (Azam), Ayoub Lyanga (Coastal Union), Abdull Aziz Makame (Yanga), Hassan Dilunga (Simba), Miraji Athuman (Simba) na Feisal Salum (Yanga).

Kikosi hichi kitaingia kambini kikiwa na kumbukumbu ya ushindi walioupata dhidi ya Kenya baada ya kutoka nao sare kwenye michezo miwili na kuwaondosha kwa mikwaju ya penati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...