Mratibu wa mshindano wa Shirika la OCCRI, Rehema Sanga akizungumza na waandishi habari kuhusiana na uratibu mashindano hayo yanayofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kivule jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SHIRIKA la Capitalizing Community and Resources Initiative (OCCRI) limeandaa mashindano ya Kivule Footbal Challenge Cup ikiwa ni lengo ya vijana kutumia fursa za maendelezo zinazowazunguka.
Mratibu wa mashindano hayo Rehema Sanga, amesema ili vijana kuweza kukutana na kuzungumza na masuala ya maendeleo ni michezo kuleta vijana kuwa sehemu moja na ujumbe kufika kirahisi.
Amesema OCCRI imeandaa mashindano ya mpira wa miguu kwa kushirikisha timu 16 za kata ya kivule na kwenye mashindano hayo washiriki watafundishwa ujasiriamali pamoja na kutumia vipaji vyao vya mpira kama sehemu ya ajira kwao.
Rehema amesema mashindano hayo yatalenga kutoa elimu ya Afya kwa vijana na kuwa na utaratibu wa kupima afya zao kila mara.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Kivule Mwanahamis Shaban ameishukuru OCCRI kwa kuleta michezo katika kata yake na kuja kwa mashindano hayo mshikamano kwa vijana pamoja na kupata fursa ya kujifunza ujasiriamali na elimu ya afya.
Amesema, dhima ya shirika hilo litachochea maendeleo kutokana na mshikamano wa michezo pamoja na utengenezaji wa fursa ajira zinazozunguka katika kata hiyo .
Mwanahamis amesema kuelekeaa uchumi wa viwanda vijana ni sehemu muhimu katika kuhakikisha dhamira ya serikali kufikia uchumi wa kati na lengo kuu ni kuona vijana wanaungana kwa kuanzisha Viwanda na kuweza kuajiri vijana wengine.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kivule, Amos Hangaya amesema kivule ina vijana wenye vipaji hivyo wakitumia vizuri wanaweza kupata ajira zinazotokana na michezo.
Katika ufunguzi wa mashindano hayo kati ya Stock City ilipata ushindi wa bao moja dhidi ya Mchikichini lililofungwa kwenye kipindi cha pili cha mchezo huo na kufanya timu hiyo kunyakua pointi tatu
Washindi katika mashindano hayo watapata fedha taslim pmaoja na vifaa vya michezo kwa mshindi wa kwanza hadi wa tatu pamoja na mfugaji bora na kipa bora wa mashindano watapata zawadi.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Kivule, Mwanahamis Shaban akizungumza namna walivyjipanga katika mashindano hayo katika kuchochea ajira katika kata hiyo.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivule, Amos Hangaya akitoa malezo namna walivyojimarisha katika sekta ya michezo katika maeneo yao.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Kivule Mwanahamis Shaban akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa mechi kati ya Stock City na Mchikichini
Mratibu wa mshindano wa Shirika la OCCRI Rehema Sanga akiwa katika picha ya pamoja na timu katika mashindano ya Kivule Footbal Challenge Cup
Mashabiki
Timu ya Stock City wakijindaa na mechi katika mashindano ya Kivule Footbal Challenge Cup
Timu ya mchikichini wakijiandaa katika mashindano ya Kivule Footbal Challenge Cup.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...