Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa –TAMISEMI,Mhandisi Joseph Nyamhanga akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo kwa Maafisa Habari na Mwasiliano wa Serikali na taasisi zake leo jijini Dodoma. Mafunzo hayo ya siku tano yaliandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao. Kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TAGCO Bi. Saraha Kibonde Msika na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Bw. Jonas Kamaleki.
Makamu Mwenyekiti wa TAGCO Bi. Saraha Kibonde Msika akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo kwa Maafisa Habari na Mwasiliano wa Serikali na taasisi zake leo jijini Dodoma. Mafunzo hayo ya siku tano yaliandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa –TAMISEMI,Mhandisi Joseph Nyamhanga akiteta jambo na Makamu Mwenyekiti wa TAGCO Bi.Saraha Kibonde Msika wakati wa hafla ya kufunga mafunzo kwa Maafisa Habari na Mwasiliano wa Serikali na taasisi zake leo jijini Dodoma. Mafunzo hayo ya siku tano yaliandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Bw. Jonas Kamaleki.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo kwa Maafisa Habari na Mwasiliano wa
Serikali na taasisi zake wakipokea vyeti vya ushiriki wa mafunzo kutoka mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa –TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo leo jijini Dodoma. Mafunzo hayo ya siku tano yaliandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa –TAMISEMI,Mhandisi Joseph Nyamhanga akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti iliyoandaa mafunzo kwa Maafisa Habari wa Serikali mara baada ya kufunga mafunzo hayo leo Jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TAGCO Bi. Saraha Kibonde Msika na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Bw. Jonas Kamaleki. Mafunzo hayo ya siku tano yaliandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao. (Picha na Idara ya Habari – MAELEZO)
Mwakilishi wa washiriki wa mafunzo kwa Maafisa Habari na Mwasiliano wa
Serikali na taasisi zake, Bw. Benton Nholo akitoa neno la shukrani kwa niaba yawenzake wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo leo jijini Dodoma. Mafunzo hayo ya siku tano yaliandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao.



*****************************



Na Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.

Maafisa Mawasiliano Serikalini wametakiwa kuitangaza miradi mbalimbali
inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano kwa wananchi.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi. Joseph Nyamhanga alipokuwa akifunga mafunzo ya siku ya tano ya Uandishi wa Habari za Serikali kwa Usahihi kwa Maafisa Mawasiliano wa Serikali, leo Jijini Dodoma.

“Serikali ya Awamu ya Tano imefanya mambo makubwa sana ikiwemo ujenzi wa barabara za lami, madaraja, reli ya kisasa, ujenzi wa vituo vya afya na hospitali,utoaji wa elimu bila malipo, ununuzi wa ndege mpya pamoja na ujenzi wa jengo la tatu la abiria Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere”.Amesema Nyamhanga.

Amesema, Maafisa Mawasiliano wanalo jukumu la kutangaza miradi hiyo na mingine mingi inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Idara (Habari) Jonas Kamaleki amesema mafunzo hayo ya siku tano yamehusisha uandishi wa kimkakati ya uandishi wa habari za Serikali kwa usahihi, namna ya kutengeneza taarifa za redio na televisheni pamoja na matumizi ya mitandao ya kijamii.

Aidha, Afisa Habari wa Halmashauri ya Bahi, Benton Nollo amesema mafunzo hayo yamekuwa muhimu sana kwao kama Maafisa Mawasiliano wa Serikali, amemuahidi Rais wa Jamhuri ya Muungano kuitangaza vyema miradi inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Chama cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali (TAGCO) kwa kushirikiana na Idara ya Habari (MAELEZO) ambapo imehusisha zaidi ya Maafisa Mawasiliano kutoka Taasisi na Idara za Serikali, Wizara, Mikoa na Halmashauri za Wilaya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...