MABINGWA wa mgumi za kulipwa nchini walioibuka na ushindi wanatarajia kushiriki katika sherehe za kupongezwa na mashabiki wao Oktoba Nne Club 361Mwenge Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwandishi wa Habari hizi Mratibu mkuu wa Pambano la kuwapongeza mabondia hao Selemani Semunyu alisema mipango imekamilika ikiwemo mabondia watakaocheza ingawa maombi ni mengi ya mabondia wengi kutaka kushiriki kuonyesha furaha yao na kuwaunga mkono mabondia hao.

Amewataja miongoni mwa mabingwa  hao ni  Abdalah Pazi ,Tonny Rashidi ,Bruno Vifua Viwili na  Nassib Ramadhani kwa pamoja na bondia yeyote binhwa na wameletea taifa heshma kubwa  wadau na mashabiki hakuna budi kuwapongeza.

" Serikali na Wabunge wamewapongeza lakini wadau na mashabiki sasa huu ndio wasaa wa kuwapongeza hata kama kuna zawadi ya kuwapa hii ndio sehemu moja lakini sie tunawapongeza kwa pambano" Alisema Semunyu.

Pambano hili pia litatumika kupata mabondia watakaowania mikanda mwezi Desemba ambapo litafanyika pambano funga mwaka.


" Watakaofanya vizuri katika pambano hili wataweza kupata nafasi katika pambano la mwezi wa 12 ambapo historia ya Ngumi nchini kwa  kipindi cha hivi karibuni utawekwa " Alisema Semunyu.

Pia amewashukuru kamisheni ya ngumi za kulipwa kutoa kibali wadhamini Smart Gin na kuomba wadhamini wengine kujitokezo kwa wingi ili kufanikisha kurejesha hadhi ya mchezo wa ngumi nchini.

Kwa upande wake mratibu wa kiufundi wa mapambano hayo Yassin Abdalah  Ustaadh aliwataja mabondia watakaosindikiza sherehe hiyo kuwa ni issa nampechehe  (Dsm) vs alli hamisi  (morogoro )

Ibrahim Makubi (Dsm)vs abdallah kingolwira  ( morogoro )Maganga kulwa (mbagala) vs Said Sudi (M'nyamala) )Hashimu msungo vs Epson john Lewis Salumu omari vs ramadhani chicho

Ameongeza kuwa mapambano yanaweza kuongezeka kutokana na  mabondia wengine kitafuta nafasi ya kutaka kishiriki Desemba lakini wengine nao wanatala kushiriki kuonuesha furaha ya ushindi huo

" Mapambano ya surprize kibao  mabingwa watakuwepo  na wasanii wa kutumbuiza njoo tuwapongeze mabondia wetu walioshinda mikanda tule tunywe tupige nao picha," alisema Ustaadhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...