Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga James Mtalitinya ameendelea kuwahamasisha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kuhakikisha wanajiunga katika vikundi ili kuweza kupata fursa ya kupewa mikopo ili kuweza kujiajiri hali itakayopelekea kupunga wimbi la wasio na ajira na hatimae kujiongezea kipato.

Amesema kuwa moja ya majukumu ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ni kutoa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu na kuongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2018/2019 halmashauri ilitoa shilingi milioni 253 na kusisitiza kuwa bado kuna milioni 32 zilizovuka mwaka ambapo kwa mwaka wa fedha 2019/2020 halmashauri inatakiwa kutoa shilingi milioni 230.

“Kufikia Mwezi wa 10 tarehe 15 tunategemea kutoa kiasi cha shilingi milino 120 ikiwa ni makusanyo ya robo ya kwanza kwa maana ya Julai – Septemba, kwahiyo tunaomba wananchi wa bangwe pamoja na wananchi wa Sumbawanga wajiunge katika vikundi visivypongua watu watano mpaka kumi halafu waainishe shughuli wanayofanya na waje waombe mkopo wa kiasi chochote, tutawakagua na baada ya hapo tutawapatia mkopo,” alimalizia.

Ameyasema hayo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo walipokuwa wakitembelea masoko yaliyopo katika mji wa Sumbawanga ili kujionea hali halisi ya maendeleo ya biashara na kujua changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo wananchi katika masoko hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...