Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme kushoto akisaidiana na baadhi ya vibarua kusafisha mahindi alipotembelea Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya chakula NFRA kanda ya Songea kuangalia zoezi la ununuzi wa mahindi linavyoendelea ambapo hadi kufikia mwishoni mwa wiki NFRA tayari imenunua tani zaidi ya 12,000 za mahindi kutoka kwa wakulima.
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme wa pili kushoto na kaimu meneja wa wakala wa Taifa wa Hifadhi ya chakula NFRA kanda ya Songea Eva Michael wa kwanza kushoto wakifanya kazi ya kusafisha mahindi yaliyoletwa na wakulima katika kituo kikuu cha kununulia mahindi eneo la Ruhuwiko mjini Songea wakati Mkuu wa mkoa alipotembelea kituo hicho kwa ajili ya kuangalia zoezi la ununuzi wa zao hilo linavyofanyika,ambapo Mkuu huyo wa mkoa alitangaza bei rasmi ya mahindi kuwa shilingi 600 kwa kilo.
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme akikusanya mahindi kabla ya kuwekwa kwenye magunia alipotembelea kituo cha kununua mahindi cha Wakala wa Taifa wa hifadhi ya chakula NFRA kanda ya Songea ambapo alitangaza kuwa Serikali kupitia NFRA kununua zao hilo kwa shilingi 600 na kuwataka wakulima wa mkoa huo kupeleka mahindi yao NFRA ili wanufaike na bei hiyo. Picha na Muhidin Amri
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...