Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU imewataka watanzania kwa ujumla kutumia uchaguzi ujao wa serikali za mitaa na vijiji vizuri pasipo kupokea RUSHWA kwa mgombea yoyote ili kuweza kuchagua viongozi bora ambao watawaongoza na kutimiza malengo yao.

Akizungumza na wanagabari jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU,Brig.Gen.John Mbungo amesema kuwa taasisi hiyo imedhamiria kuwaelimisha wananchi ili waweze kuchagua viongozi ambao wataendelea yale yote mema yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tano.

“Ni dhamira ya TAKUKURU kuona kwamba umakini unakuwepo kuchagua viongozi waadilifu, wazalendo na wasiojihusisha na vitendo vya Rushwa unazingatiwa na watanzania wote katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa na vijiji utakofanyika Novemba mwaka 2019”. Amesema Brig. Gen. Mbungo.

Aidha,Brig.Gen.Mbungo amesema kuwa uelimishaji unafanyika nchi nzima ,jitihada zimefanyika ili kuzitumia Rdio za jamii ambazo zipo katika mikoa mbalimbali nchini ambako TAKUKURU inazo ofisi zake.

“Njia nyingine ya uelimishaji tunayoitumia ni kupitia maonesho ya filamu katika mikusanyiko mbalimbali ikiwemo mikesha ya mbio za Mwenge wa Uhuru unaokimbizwa nchi nzima hadi Oktoba 14,2019.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...