Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

RAIS wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amezitaka Wizara zinazoshughulika na masuala ya ulinzi na usalama kuhakikisha wanaangaza katika matukio ya kikatili yaliyowalenga wageni nchini humo ikiwa ni pamoja na kukomesha kabisa matukio hayo.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Ramaphosa ameandika kuwa hakutakuwa na uhalali kwa raia wa Afrika kusini kuwadhuru watu kutoka nchi nyingine za Afrika na kueleza kuwa watu nchini humo wanatakiwa kuishi kwa amani hata kama kuna shida yoyote inatakiwa kumalizwa kwa kufuata misingi ya Kidemokrasia.
 

Kwa upande wa balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Richard Lupembe amesema kuwa hadi leo mchana hakuna tukio lolote la raia wa Tanzania kudhurika kwa namna yoyote katika vurugu hizo zilizowalenga wageni.

Chombo cha habari Cha Aljazeera kimeripoti kuwa katika mitaa ya Alexandra polisi walionekana wakidhibiti kikosi cha watu 50 waliokuwa wanarusha mawe.
Vurugu hizo ziliibuka jumatatu wakati vikosi vya uokoaji vikizima moto katika jengo la Jeppestown ambapo iliripotiwa kuwa watu kadhaa walipoteza maisha na majeruhi walipatikana, watu katika vikundi mbalimbali waliendeleza kuvamia sehemu za biashara na kuchoma moto na kupora huku ikielezwa kuwa waliathirika zaidi ni raia kutoka nchi za Nigeria, Somalia na Ethiopia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...