Mafundi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga UWASA) wakiwa kazini kama wanaavyooekana
  Fundi kutoka Idara ya Ufundi Tanga Uwasa Kitengo cha  Maji Taka Sikujua Shabani  wa pili kutoka kulia akionyeshwa kitu na mafundi
 Eneo la barabara ya sita ambapo bomba limeharibika lenyewe kutokana na udhaifu maji yamepita mengi na limeshindwa  kuhimili msukumo wa maji.
 Meneja Ufundi wa Mamlaka ya Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga UWASA)  Mhandisi Rashidi Shaban akizungumza na waandishi wa habari leo


MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga UWASA)   wameeleza sababu za uwepo wa changamoto ya mtandao wa majitaka inatokana na  uchakavu wa  mabomba kuwa yamelazwa siku nyingi  na mengi yakiwa ya zege na udongo. 

Changamoto imesababisha uzibaji na utirishaji wa majitaka katika  baadhi ya maeneo ya makazi hivyo kusababisha malalamiko kwa wateja.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Meneja Ufundi wa Mamlaka hiyo  Mhandisi Rashidi Shabani alisema Tanga Uwasa imejipanga kutatua changamoto  hiyo kwa kufanya ukarabati kwa awamu katika maeneo korofi ili kuondoa kero hiyo.

Changamoto ya mfumo wa majitaka imeonekana katika eneo la barabara ya sita na ishirini ambapo ilisababishwa na kubanjika kwa bomba hilo kutokana na  msukumo mkubwa wa maji hivyo kupelekea mafuriko ya majitaka kwa maeneo  mengine. kuna bomba limeharibika lenyewe kutokana na udhaifu maji mengi  kupita na limeshindwa kuhimili msukumo wa maji hayo.

Alisema kwamba tatizo hilo limekutokana na umri wa mabomba hayo yaliyopo  ardhini mengi yamekuwa mabovu na hayawezi kuhimili maji mengi  kunakosababiswa na watu kuongezeka maji yanayopita kwen ye mtandao huo  yamekuwa mengi kulinganisha na uwezo wa kuhimili mabomba hayo kutokana umri  yaliyokwa nayo

Mhandisi Shabani alisema kwenye eneo la barabara ya sita kuna bomba  limeharibika lenyewe kutokana na udhaifu maji yamepita mengi na limeshindwa  kuhimili msukumo wa maji.

“Hivyo sisi kama Tanga UWASA tumejipanga kufanya ukarabati tayari kijiko  kipo eneo la tukio kimeshaanza uchimbaji huku akiwaomba wananchi  wawavumilie ndani ya siku mbili kwenye eneo la barabara kwa sababu ya  kufanyia huo ukarabati”Alisema

Alisema kwamba wanaamini ndani ya siku mbili zijazo takuwa wamemaliza kazi
kubwa eneo hilo

“Lakini pia tutatumia ndani ya siku saba a au nane kukamilisha huduma hii hivyo wananchi wanaotumia barabara hii wapite pembeni kwa sababu hiyo ni  hatari kwa afya zao kutokana na maji taka”Alisema

Naye kwa upande wake fundi kutoka Idara ya Ufundi Tanga UWASA kitengo cha  Maji Taka Sikujua Shabani alisema tatizo lilpotokea mara moja wameanza kazi  kwani maji taka yanapomwagika ni athari kwa wananchi.

Hata hivyo alisema kwamba wameendalea kuwaelimisha wananchi kuwa wavumilivu  kwani wao hivi sasa wanalishughulikia tatizo hilo ili hali yake iweze  kurudi kawaida.

mwisho

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...