Wachezaji Kutoka kulia Merci Nyanchama wa Kenya Peace Kabasweka wa pili kulia wakibadilishana matokeo na Angel Eaton wakwanza Kushoto na Hawa Wanyenche wa Pili Kushoto wote wa Lugalo mara baada ya kumaliza mchezo kwa Siku ya pili ya mashindano ya wazi ya Wanawake Tanzania katika Uwanja wa TPC Moshi (Picha na Luteni Selemani Semunyu).

Wachezaji Merci Nyanchama wa Kenya na Peace Kabasweka kulia na Angel Eaton na Hawa Wanyenche kushoto wa Lugalo wakipongezana mara baada ya kumaliza mchezo kwa Siku ya pili ya mashindano ya wazi ya Wanawake Tanzania katika Uwanja wa TPC Moshi (Picha na Luteni Selemani Semunyu).

********************************

Na Luteni Selemani Semunyu

Mashindano ya golf ya wanawake Tanzania yamefikia siku ya pili huku wachezaji kutoka klabu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo wakichuana vikali na mchezaji kutoka Uganda Peace Kabasweka.

Mchezaji huyo wa Uganda aliongoza tangu siku ya kwanza kwa fimbo mbili dhidi ya Angel Eaton wa Lugalo akifuatiwa na Hawa Wanchenche wa Lugalo pia.

Licha ya kuongoza kwa fimbo mbioli siku ya kwanza mchezaji huyo kutoka uganda alisema bado mchezo ni mgumu na matumaini ya kuibuka na ushindi bado ni magumu na mwamuzi ni siku ya mwisho ya mchezo

“ Wachezaji kutoka Lugalo ni Wakali na Wanajituma na Idadi ya Fimbo ninazoongoza ni chache hivyo ukifanya mzaha kidogo basi ni rahisi kufungwa hivyo bado naweza kusema Mchezo ni Mgumu” Alisema Kabasweka

Naye Mchezaji kutoka Lugalo Angel Eaton aliyekuwa akimfuatia alisema peace ni Mchezaji mzuri na mchezo bado uko upande wake lakini hakuna kukata tamaa mpaka dakika ya mwisho.

“ Nimetumwa na klabu yangu ushindi hivyo nitapambana kuhakikisha ubingwa unakwenda lugalo mengine tumwachie mungu kwani kuna wachezaji wazuri tu na wanacheza vizuri mpaka sasa “ Alisema Angel.

Kwa Upande wake mchezaji Hawa Wanchenche naye kutoka kutoka klabu ya Lugalo alisema wamepangwa kundi moja leo kutokana na mchezao mzuri na hapa tunawania ubingwa lakini pia nafasi kushiriki mashindano nchini Uganda.

Kutoka Kenya ambao nao wameshiriki katika mashindano haya mchezaji Merci Nyanchama kutoka kwa upande wake alisema amecheza vibaya hivyo hana matumaini ya ushindi lakini kiujumla mashindano ni mazuri na yamevutia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...