Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv
MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema kutokana na ubora wa huduma zao, umevutia wageni  kutoka nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Akizungummzia ubora wa huduma zao leo Septemba 18,2019, Kaimu Meneja wa Huduma za Utabiri TMA, Wilberforce Kikwasi amesema kutokana na taarifa zao kuwa na ukweli wa zaidi ya asilimia 80, kumekuwa na kasi kutoka kwa wataalam wa hali ya hewa kutoka SADC wanaotembelea banda la mamlaka hiyo.

Amesema  katika mkutano huo watawaonyesha wataalamu wenzao  namna wanavyofanya kutafuta, kuchakata na kutoa taarifa za hali ya hewa kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Kikwasi, TMA pia imepata uzoefu kwenye mkutano huo kwa nchi zinazopata majanga yanayotokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

"Nchi yetu inatumika kimkakati katika ukanda huu na hii ni kutokana na miundombinu tuliyonayo ambayo serikali imetusaidia sana. Wananchi hapa nchini wana nafasi kubwa ya fursa za kiuchumi kwa kufuatilia na kuzitumia taarifa za hali ya hewa," amesema Kikwasi.

Ameongeza kuwa biashara  zinategemea sana taarifa za hali ya hewa na shughuri nyingine pia za kimaendeleo hivyo, TMA inawashauri wananchi wafuatilie taarifa wanazozitoa.

Amesema maendeleo ya wakati ujao kwa Tanzania, SADC na nchi zote za Afrika zinategemea zaidi taarifa za hali ya hewa hivyo wadau na wananchi kwa ujumla wanapaswa kuzifuatilia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...