Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura ya Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) upande wa Habari  Daniel Kasokola (katikati ya wanafunzi) akieleza jambo kuhusu watu wenye ulemavu wakati Gari la Matangazo la NEC lilipotembelea Shule ya Sekondari ya Rugambwa iliyopo Manispaa ya Bukoba kutoa Elimu ya Mpiga Kura kuelekea Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mkoa wa Kagera, Kigoma na Wilaya ya Chato unaoanza Oktoba 2 hadi Oktoba 8, 2019. 
 Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura ya Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) upande wa Habari  Daniel Kasokola (katikati) akifafanua nafasi ya watu wenye ulemavu katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura akiwa na baadhi ya wanafunzi wenye ulemavu wanaosoma Shule ya Sekondari ya Rugambwa ya Manispaa ya Bukoba.
 Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura ya Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) upande wa Habari  Daniel Kasokola (kulia mwenye fulana nyeusi) akifafanua jambo mbele ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Rugambwa ya Manispaa ya Bukoba.
 Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Yasinta Mlula akiwaeleza jambo wakazi wa Manispaa ya Bukoba wakati Gari la Matangazo la Tume lilipokuwa likitoa Elimu ya Mpiga Kura kwenye Stendi ya Mabasi ya Mjini Bukoba kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
  Mkazi wa Manispaa ya Bukoba mwenye ulemavu akiwa na Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Ibrahim Dedu wakati Gari la Matangazo la Tume (halipo pichani) lilipokuwa likitoa Elimu ya Mpiga Kura kwenye Stendi ya Mabasi ya Mjini Bukoba kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
 Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Christina Njovu akimweleza jambo mkazi wa Manispaa ya Bukoba mwenye ulemavu wakati Gari la Matangazo la Tume lilipokuwa likitoa Elimu ya Mpiga Kura kwenye Stendi ya Mabasi ya Mjini Bukoba kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
 Gari la Matangazo la Tume ya Taifa ya Uchaguzi likipita karibu na Stendi ya Mabasi ya Mjini Bukoba kutoa Elimu ya Mpiga Kura ikiwa ni maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mkoa wa Kagera, Kigoma na Wilaya ya Chato unaoanza Oktoba 2 hadi Oktoba 8, 2019.
 Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura ya Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) upande wa Habari  Daniel Kasokola akizungumza na wakazi wa Manispaa ya Bukoba wakati Gari la Matangazo la Tume lilipoweka kambi kwenye eneo la wazi katika Manispaa ya Bukoba kutoa Elimu ya Mpiga Kura.
 Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Monica Wabukundi, akiwasiliza vijana kwenye Stendi ya mabasi ya Mjini Bukoba wakati Gari la Matangazo la Tume lilipokuwa likitoa Elimu ya Mpiga Kura kwenye stendi hiyo kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Moshi Makuka (mwenye fulana nyeupe karibu na Gari la Matangazo) akitoa Elimu ya Mpiga Kura kwenye moja ya mitaa ya Mjini Bukoba akiwa na Gari la Matangazo la Tume kuhamasisha wananchi kujitokeza kwenye kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mkoa wa Kagera, Kigoma na Wilaya ya Chato unaoanza Oktoba 2 hadi Oktoba 8, 2019. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...