Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akimkabidhi
kadi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mmoja wa wananchi aliyejiunga na
CCM akitokea chama cha upinzani.



Mkuu wa Wilaya ya Newala, Mhe. Aziza A. Mwangosongo akizungumza na
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wilayani Newala wakati wa
Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
yaliyofanyika wilayani humo jana na kuwahimiza wananchi kufanya
maandalizi mapema ya kuwanunulia vifaa vya shule watoto waliohitimu
darasa la saba.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akizungumza
na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) (hawapo
pichani) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Wanawake
Tanzania (UWT) yaliyofanyika jana wilayani Newala.

Baadhi ya wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wilayani
Newala wakimsiliza Mgeni Rasmi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe.
George H. Mkuchika (Mb) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa
Wanawake Tanzania (UWT) yaliyofanyika wilayani humo jana.
*********************************

Na James K. Mwanamyoto, Newala

Wanawake nchini wametakiwa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali katikauchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 24 Novemba,2019 kwani wana nafasi kubwa katika mchango wa maendeleo ya Taifa.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishiwa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) ambayealikuwa mgeni rasmi wa Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa WanawakeTanzania (UWT) wilayani Newala.

Mhe. Mkuchika amewaasa wanawake nchini, kutotegemea nafasi za upendeleowalizotengewa na Serikali na badala yake wachukue fomu na kuingia katikakinyang’anyiro na wanaume kugombea nafasi zilizotangazwa kwa mujibu wakanuni zinazosimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

“Serikali ya kijiji ndio inayozungumzia suala la maendeleo ya kijiji, hivyo kijijiambacho hakina zahanati, mjumbe mwanamke ni hodari wa kukumbusha ujenziwa zahanati kwani anatambua umuhimu wa zahanati”, amefafanua Mhe.Mkuchika.

Mhe. Mkuchika amesema Serikali inataka wanawake washiriki katika vikao vyaSerikali ya kijiji na mtaa ili wawe chachu ya mafanikio katika vijiji na mitaa, kwaniwananchi katika maeneo hayo wanahitaji kupata huduma bora toka Serikalini.

Mhe. Mkuchika ametoa hamasa kwa kina mama kuwa mstari wa mbele
kuwahimiza akina baba kutekeleza ahadi waliyoitoa ya kuchangia chakula chawatoto wa shule ili kuwawezesha watoto hao kusoma vizuri pasipo kukabiliwa nachangamoto ya njaa.

Aidha, Mhe. Mkuchika ametumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi mafanikio yayaliyoletwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika sekta ya afya kwa kujengahospitali za wilaya nchini.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufulitangu aingie madarakani amejenga hospitali nyingi za wilaya kuliko alizozikuta,kwani amedhamiria ndani ya utawala wake kila wilaya nchini iwe na hospitaliyake na ushahidi wa wazi uko katika Wilaya ya Newala ambayo imenufaika naujenzi wa kituo cha afya cha Mpunye na Kitangali”, amesema Mhe. Mkuchika.

Mhe. Mkuchika ameongeza kuwa, kwa upande wa ujenzi wa barabara, mara
baada ya Serikali kuweka lami, wananchi wameweza kusafiri kwa muda mfupikutoka mkoa mmoja kwenda mwingine akitolea mfano wa abiria wanaosafiri kwamabasi kutoka Mbinga na Newala kwenda Dar es Salaam wamekuwa wakitumiasiku moja badala ya siku mbili kama ilivyokuwa huko nyuma, halikadhalika naKutoka Lindi kwenda Dar es Salaam mabasi yamekuwa yakiondoka asubuhi nakurudi siku hiyo hiyo.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza A. Mwangosongo amempongezaMhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa elimu bure kwa watoto ambaondio taifa la kesho na amewataka wazazi wa wanafuzi waliohitimu darasa lasaba wilayani humo kuunga mkono azma ya Mheshimiwa Rais kwa kufanyamaandalizi mapema ya kuwanunulia vifaa vya shule ikiwepo sare za shulewatoto wao ili waweze kunufaika na elimu ya sekondari inayotolewa bure naSerikali.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT) ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Bi. Zainabu Msuweta amemshukuruMhe. Mkuchika kwa nasaha zake na kuahidi kuwa UWT itazifanyia kazi ili ziwezekuwa na manufaa kwa wanawake wilayani Newala.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na UtawalaBora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) amepata mwaliko wa kuwaMgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT) wilayani Newala, wakati akiwa mkoani Mtwara kwenye ziara yake yakikazi ya kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma mkoani humo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...