Wimbo mpya wa JAMAFEST2019 ulioimbwa na Msanii Peter Msechu, umeteuliwa kuwa wimbo maalum katika Tamasha la Utamaduni la Afrika Masharikilinalotarajiwa kufanyika nchini kuanzia Septemba 21-28 mwaka huu katika Uwanjawa Taifa Jijini Dar es Salaam.

Taarifa za wimbo wa JAMAFEST2019 kuteuliwa kuwa wimbo rasmi wa Tamasha hilomaarufu Afrika Mashariki zilifahamika baada ya Msechu kuandika katika ukurasawake wa Instagram akimshukuru Mungu kwa wimbo wake huo kupitishwa.

Akiongea baada ya kupigiwa simu kutoa ufafanuzi juu ya kuchaguliwa kwa wakekuwa kuwa maalum katika tamasha la JAMAFEST, Msechu alisema kuwa alitungawimbo huo baada ya uongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezokuwaomba wasanii mbalimbali kutunga wimbo ambao ungetumika kama wimbomaalum wa Tamasha.

“Wasanii tupo wengi sana kwa mimi kupata fursa hii ya kuimba katika ufunguzitamasha hili kubwa la JAMAFEST kwangu ni heshima kubwa sana. Tulikuwa wasaniiwengi tuliotunga nyimbo kwa ajili ya Tamasha lakini wimbo wangu umechaguliwani furaha kubwa”, alieleza Msechiu.

Amesema kwa sasa anaandaa video ya wimbo huo ili uweze kutumika kuhamasishawatanzania na watu wa Afrika Mashariki kushiriki katika Tamasha ambalo lengo lakudumisha uridhi wa utamaduni, Sanaa za mikono na ubunifu, biashara na kukuzaAkiongea kuhusiana na Wimbo huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi ya Tamasha la JAMAFEST, Bi. Joyce Fissoo alisema kuwa mchakato wa uteuzi wa wimbo rasmi kwa ajili ya Tamasha la JAMAFEST haukuwa rahisi kwani kulikuwa na ushindani mkubwa kutokana na wasanii wengi wakujitokeza na kufanya utunzi wawimbo kwa ajili ya tamasha .

“Mchakato wa kupata wimbo wa Tamasha ulikua mgumu kutokana na wasaniikujitokeza na baada ya kusikiliza nyimbo zote ndipo Sekretarieti ya Maandalizi yaTamasha inayoundwa na Wajumbe kutoka nchi sita wanachachma wa Jumuiya yaAfrika Mashariki ikauchagua wimbo wa JAMAFEST2019 ulioimbwa na Msechu kuwandio wimbo wa tamasha”, alieleza Bi. Fissoo.

Tamasha la JAMAFEST ni tamasha lililopitishwa na Baraza la Mawaziri la Jumuiya yaAfrika Mashariki ili kuenzi na kulinda utamaduni wa makabila ya Afrika Mashariki.Tamasha hili hufanyika kila baada ya miaka miwili katika nchi wanachama ambapomwaka huu tamasha hilo litafanyika nchini Septemba 21-28 katika Uwanja waTaifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...