KAMPUNI ya Star Media, Shirika la mtandao wa China pamoja na Wizara ya habari, utamaduni, Sanaa na michezo wamezindua rasmi mahusiano ya kushirikiana kubadilishana tamaduni kupitia mtandao na hiyo ni kwa kupitia filamu na tamthiliya mbalimbali.
Akizungumza katika hafla hiyo Mtendaji Mkuu wa Shirika la Mtandao la China Zhao Hui amesema kuwa mahusiano ya baina ya Tanzania na China yamekuwa yakiimarika kila siku huku wakishirikiana zaidi katika masuala ya tamaduni huku mahusiano ya China na Afrika yakiendelea kukua na kudumu kila siku.
Amesema kuwa mtandao umekuwa ukiwaweka watu karibu zaidi tofauti na ilivyokuwa awali na wanaamini azma hiyo ya kubadilishana tamaduni baina ya nchi hizo mbili utakuza mawasiliano pamoja na mawasiliano.
Pia katibu wa kwanza wa Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini amesema mahusiano ya China na Tanzania yamezidi kukua zaidi na hiyo ikiwa ni matokeo bora yaliyopandwa na waasisi wa mataifa hayo ambao walipanda mbegu bora ya ushirikino, ambayo matokeo yake yanaonekana sasa hivi.
Amesema mahusiano kupitia mtandao utaimarisha mahusiano ya nchi hizo mbili huku akipongeza idadi kubwa ya wanafunzi wanaojifunza lugha ya kichina katika vituo vya Chuo kikuu cha Dar es Salaam na Chuo kikuu cha Dodoma.
Amesema wanafunzi hao wanaojifunza lugha hiyo wamekuwa wakitembelea nchi hiyo ili kuweza kujifunza zaidi ili kuendelea kujifunza na kudumisha mahusiano hayo yaliyodumu kwa miaka 55 sasa.
Kwa upande wake mchekeshaji maarufu nchini Ebitoke amesema kuwa mitandao ya kijamii ina nguvu sana hivyo haina budi kuitumia vizuri ili kuwezesha zaidi masuala ya kibiashara na mahusiano bora baina ya China na Tanzania.
Amesema kuwa mtandao mahusiano bora baina ya China na Tanzania yataimarika zaidi pamoja na kuelewana miongoni mwao na hiyo ni sambamba na kuendeleza mahusiano katika masuala ya biashara, elimu na tamaduni.
Wadau
mbalimbali wa serikali ya China, Tanzania na mitandao wakikata utepe
kuashiria uzinduzi rasmi mahusiano ya kushirikiana kubadilishana
tamaduni kupitia mtandao uliofanyika leo katika Hoteli ya Serena Jijini
Dar es Salaam.
Mtendaji
Mkuu wa Shirika la Mtandao la China Zhao Hui akizungumza kuhusu
mahusiano ya Tanzania na China katika masuala ya elimu, miundombinu na
kushirikiana katika tamaduni wakati
wa uzinduzi rasmi wa mahusiano ya kushirikianakatika kubadilishana
tamaduni kupitia mtandao uliofanyika leo katika Hoteli ya Serena Jijini
Dar es Salaam.
Katibu
wa kwanza wa utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania, Zhang
Bing akizungumza kuhusu namna ushirikiano wa Tanzania na China
ulivyoweza kuunganisha tamaduni za nchi hizo mbili wakati wa uzinduzi
rasmi mahusiano ya kushirikiana kubadilishana tamaduni kupitia
mtandao uliofanyika leo katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Mchekeshaji
kwenye Mitandao ya kijamii Anastazia Exavery maarufu kama Ebitoke
akizugumza kuhusu namna mitandao ya kijamii ilivyoweza kuinua kipaji
chake wakati wa uzinduzi rasmi mahusiano ya kushirikiana kubadilishana
tamaduni kupitia mtandao uliofanyika leo katika Hoteli ya Serena Jijini
Dar es Salaam.
Mchekeshaji
kwenye Mitandao ya kijamii Agness Joseph, Maye Kidoti akizungumzia
mafanikio aliyoyapata kupitia mitandao ya kijamii wakati wa uzinduzi
rasmi mahusiano ya kushirikiana kubadilishana tamaduni kupitia
mtandao uliofanyika leo katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Wadau
mbalimbali wa masuala ya utamaduni wa Tanzania na China wakiwa kwenye
ukumbi wa mkutano wakati wa uzinduzi rasmi mahusiano ya kushirikiana
kubadilishana tamaduni kupitia mtandao uliofanyika leo katika Hoteli ya
Serena Jijini Dar es Salaam.
Wadau
mbalimbali wa serikali ya China, Tanzania na mitandao wwakiwa kwenye
picha ya pamoja wakati wa uzinduzi rasmi mahusiano ya kushirikiana
kubadilishana tamaduni kupitia mtandao uliofanyika leo katika Hoteli ya
Serena Jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...