Na Ripota Wetu,Michuzi TV

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam Daniel Chongolo amefanya ziara katika Kata ya  Mbezi Juu kwa lengo la kujionea utekelezaji wa utatuzi wa changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wa eneo hilo.

Akizungumza akiwa katika Kata hiyo leo Oktoba 8, 2019  Chongolo amesema amefanikiwa kuona kinachoendelea kwa sasa katika kutatua changamoto ya maji kwa wananchi wa Mbezi Mtoni na maeneo yanayozunguka eneo hilo.

" Tumekubaliana na DAWASA Kawe kushughulikia changamoto hizo kwa haraka, nami baada ya wiki mbili nitarudi tena kuangalia maendeleo ya kazi ya kuwafikishia maji wananchi. Lengo la Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Jemedari wetu Rais John Magufuli ni kuhakikisha kuwa wanaKinondoni wote wanapata maji safi na salama ifikapo 2020,"amesema

Ameongeza kuwa mpaka sasa tupo zaidi ya asilimia 80 na kuongeza matanki matano yamekamilika na kila moja lina uwezo wa kihifadhi lita milioni sita." Mungu ni mwema, kwani ni hakika mama wa Kinondoni ikifika 2020 atasahau kubeba ndoo ya maji kichwani,".
 MKUU wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam Daniel Chongolo akielezwa jambo kutoka kwa mmoja wa Wafanyakazi wa DAWASA Kawe, akiwa kwenye ziara yake katika Kata ya  Mbezi Juu kwa lengo la kujionea utekelezaji wa utatuzi wa changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wa eneo hilo.
 MKUU wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam Daniel Chongolo akimsikiliza mmoja wa Wananchi wanaoishi katika eneo hilo la Mbezi Juu kuhusu changamoto ya upatikanaji wa maji kwa Wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...