Mzee William Lobulu alizaliwa 20 Desemba 1951 Sanawari, Arusha.

Alifanya kazi Shirika la Habari Tanzania (SHIHATA) baada ya kuhitimu Shahada ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadaye alipata Shahada ya Uzamivu Chuo Kikuu cha Meriland, Marekani alipokuwa  Mkufunzi katika Chuo cha Uandishi wa Habari Tanzania, (TSJ).

Alifanya kazi za uandishi wa habari, uhariri pamoja na kuchapisha gazeti la "Arusha Times".

Pia alifanya kazi ya ushauri yaani "consultancy" inayohusiana na masuala ya machapisho katika mashirika ya mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Marehemu alibatizwa kanisa la KKKT Ilboru. Alifunga ndoa ambayo ilibarikiwa Kanisa la KKKT Mjini Kati mwaka 1986. Mzee William ameacha mke na watoto watatu na mjukuu mmoja. 

Alikuwa akisumbuliwa na asthma ambayo ilimshika ghafla na taa yake ikazima alipoitwa mbinguni saa 12 asubuhi Jumapili tarehe 6 Oktoba 2019.

Familia inatoa shukrani kwa wote waliohusika kumhudumia marehemu kwa hali na mali kuhusiana na afya yake.

Tunashukuru Wachungaji, Wainjilisti na Wazee wa Kanisa na watumishi wote waliokuwa wakimpa huduma mbalimbali za kiroho.

Marehemu atakumbukwa kwa ushirikiano, upole, ucheshi na moyo wa huruma kwa watoto na watu wote kwa ujumla. 

BWANA ametoa, BWANA ametwa jina la BWANA lihimidiwe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...