
Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Elias Kwandikwa akichomelea chuma kuashiria kuanza kwa ujenzi wa kivuko kipya cha Mafia Nyamisati. Kivuko hicho kitakuwa na uwezo wa kubeba abiria 200 na magari 6 sawa na tani 100, kinajengwa kwa shilingi bilioni 5.3 za Kitanzania na kitakamilika ifikapo mwezi Februari mwakani.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Maselle kushoto akisoma taarifa fupi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mheshimiwa Mhandisi Elias Kwandikwa wa (pili kushoto)wakati alipokua akizindua ujenzi wa kivuko kipya cha Mafia Nyamisati, tukio lililofanyika katika yadi ya Songoro Kigamboni. Kutoka kulia ni Lazaro Vazuri na mbunge wa Mafia Mbaraka Dau.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...