Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabenki Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kulia) akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Anold Kihaule (wa pili kushoto) alipomtembelea ofisini kwake na kujadili jinsi ya kuweza kuunganisha nguvu za upatikanaji wa vitambulisho vya Taifa kwa urahisi ili vitumike kwenye utambulisho wa kufungulia akaunti za Benki. Kwa mujibu wa Bwana Nsekela, vitambulisho vya Taifa ni nguzo muhimu sana katika zoezi la ufunguaji akaunti kwa wateja kwani vinabeba taarifa zote za utambuzi zinazohitajika na mabenki. Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa TBA, Tuse Joune (kushoto) na Mkurugenzi wa Tehama wa NIDA, Gideon Ndalu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...