Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John  Pombe Magufuli akiongea kwa simu na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro na kumuagiza kumsimamisha kazi mara moja Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Sumbawanga ACP Polycarp Urio kwa kutowasilisha taarifa kwa Mkuu wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa  maelekezo ya Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Kangi  Lugola ambaye hivi karibuni aliagiza kuhamishwa kituo cha kazi askari polisi Tisa waliokuwa wakijihusisha na vitendo vya rushwa na kuwabambikizia kesi wananchi. Mhe. Rais alitoa maagizo hayo alipotembelea Kituo cha Polisi cha Laela mara baada ya kuzindua rasmi Barabara ya Tunduma-Laela-Sumbawanga yenye urefu wa kilometa 223.2 ambayo ni sehemu ya barabara kuu katika ushoroba wa Magharibi unaoanzia Tunduma-Mpanda-Kigoma-Nyakanazi wenye urefu wa kilometa 1,286.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...