Serikali imesema ipo tayari kulipa Deni la shilingi Bilioni 13 kwa wakulima wa korosho  Wilayani Tandahimba.

Hayo ameyasema Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumbo wakati akijibu maswali na kusikiliza kero mbalimbali za  wananchi wa Kijiji Cha Nachunyu 

"Msema kweli mpenzi wa Mungu,tulishindwa kuendelea kuwalipa kwakuwa fedha ilituishia,lakini Sasa tumeshapata fedha baada ya kuuza korosho zetu zote tan220,000  kwaiyo fedha tunayo tunauhakika wa kuwalipa wakulima,"alisema Mgumbo

Alisema  serikali inatarajia kulipa madeni kwa wakulima na vibarua Tanzania nzima shilingi Bilioni 89  ambazo zipo.

"Utaratibu utafanyika katika malipo hayo lakini fedha kwa Sasa ipo,sababu tulikuwa tunalipwa kwa malipwani yaani mzigo upakiwe kwenye meli ndipo malipo  yafuaate kwaiyo tumemaliza zoezi hilo ," alisema Mgumbo

Aidha alisema maghala yapo wazi tayari kwa kupokea mzigo mpya hivyo muda wowote  wataanza kupokea korosho kutoka kwa wakulima
 Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumbo na Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba akipata maelezo kutoka kwa mkulima Ahmad Ulenje
Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumbo  akifafanua jambo wakati akijibu maswali na kusikiliza kero mbalimbali za  wananchi wa Kijiji Cha Nachunyu 
,kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...