Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Utegi Enterprises (T)LMT Otieno Igogo (kulia) akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu  udhamini wa michuano ya mchezo wa mpira wa miguu kuelekea katika maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Hayati Mwalimu Julius Nyerere Octobar 14 mwaka huu.Kushoto ni Mratibu wa  mashindano hayo Shaban Mparure.

Na Said Mwishehe, Michuzi TV
 TIMU 14 kutoka Kata ya Msigani Kinondoni jijini Dar es Salaam zimefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya kuwania kombe la kumbukumbu ya kifo cha Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

 Kwa mujibu wa waandaaji wa mashindano hayo yaliyoanza Septemba 14 mwaka huu kwa kuwa na  timu 48 na kwamba timu ambazo zimeingia hatua ya nusu fainali  ambayo itaanza kutumia vumbi kuanzia Jumamosi ya wiki ijayo.

Katika kuhakikisha ushindani unakuwa mkubwa kwenye michuano hiyo Zawadi za vikombe na medani zitatolewa katika  timu ambazo zitashika nafasi ya kwanza na ya pili ambapo timu hizo zitafanyika katika makundi matatu na kila kundi linatimu nne.

Akizungumza zaidi leo Oktoba 4 ,mwaka huu jijini Dar es Salaam  mmoja wa waandaaji wa  mashindano hayo Shaban Mparure amesema katika kuhakikisha michuano inakuwa na ushindani walishirikisha timu  hizo 48 na timu  12 kati ya hizo ndio zimefanikiwa kuingia  hatua hiyo ya  nusu fainali.

Amesema kuwa mashindano hayo yamedhaminiwa na Mwenyekiti Mtendaji  wa kampuni ya UTEGI Techical Enterprises (T) LTD Otieno Igogo ambaye ndio ametoa vikombe na zawadi mbalimbali kwa ajili ya kudhamini Mashindano hayo ya  kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.

Mparure amesema fainali za mashindano hayo zinatarajia kufanyika katika Uwanja wa  wa Uhuru jijini Dar es Salam kuazia Oktoba nane hadi Oktoba tisa na kwamba  kadri siku zinavyozidi kwenda watatoa ratiba kamili ya fainali hizo.

Kuhusu zawadi za washindi amesema mshindi wa kwanza atapata  Kombe kubwa na mpira mmoja na  zawadi wa mshindi wa pili itakuwa mpira mmoja.Pia kutakuwa na zawadi ya mchezaji bora.

Mparure amesema  lengo kubwa la kufanya mashindano hayo ni mwendelezo wa  kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere ambaye alikuwa mpenda michezo na mzalendo wa nchi yake na Afrika kwa ujumla.

Awali akizungumzia udhamini wake Mwenyekiti huyo wa Kampuni ya Utegi interprises (T) LTD Otieno Igogo  amesema kuwa Mwalimu  alikuwa zawadi ya pekee  kwa ajili ya kuikomboa Afrika na mzalendo wa nchi yake na kwamba alihamasisha watu kuwa katika misingi hiyo pia aliweza kuunganisha nchi katika misingi ya umoja wa kitaifa.

Igogo amesema kwamba Nyerere alijenga misingi mizuri ya kikatiba na uhuru wa habari pia aliruhusu uwepo wa  mfumo wa vyama vingi na msingi mzuri wa kielimu.

Igogo amesema wao kama Kampuni wamejikita kwenye biashara ya forodha na zaidi ya miaka 35 ana endelea na kazi hiyo kuazia Mwaka 1984 .na amekuwa alifanya kwa nidhamu kubwa mno ikiwamo kulipa stahiki zote za Serikali.

Ameongeza kuwa yote ambayo anaya fanya ni katika kuendelea kumuenzi Mwalimu Nyerere na hasa kwa kutambua Oktoba 14 mwaka huu Watanzania tuna adhimisha miaka 20 ya kukumbuka ya kifo chake.

Amesema  ni matumaini yake kupitia mashindano hayo ya kumuenzi Mwalimu Nyerere vijana watapa nafasi ya kutambua mchango wa Mwalimu katika kuhakikisha  nchi yetu inakuwa na umoja,upendo na mshikamano na leo hii hakuna anayezingumzia ukabila wala udini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...