Zoezi la kuutafuta mwili wa Samwel Gilda Mhina( 29)anayesadikiwa kupotea katika ziwa Momela mara baada ya kuzama kwa mtumbwi Katika kijiji cha Olkungwando ,kitongoji cha Momela kata ya Ngarenanyuki ,Tarafa ya King’ori wilyani Arumeru.
Zoezi la kuutafuta mwili wa Samwel Gilda Mhina( 29)anayesadikiwa kupotea katika ziwa Momela mara baada ya kuzama kwa mtumbwi Katika kijiji cha Olkungwando ,kitongoji cha Momela kata ya Ngarenanyuki ,Tarafa ya King’ori wilayani Arumeru.
Zoezi la kutafuta mwili likiendelea kama linavyoonekama katika picha katika ziwa Momela
Na.Vero Ignatus,Arusha.
Mtalii raia wa Ujerumani aliyefahamika kwa jina la Rosenbever Heike,pamoja na nahodha wa mtubwi Samwel Gelda Mhina( 29)wamezama katika Ziwa Momela ambapo mtalii huyo alifanikiwa kujiokoa huku juhudi za kutafuta mwili wa nahodha huyo zikiendelea.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamishna Msaidizi wa Polisi mkoa wa Arusha Koka Moita amesema tukio hilo lilitokea majira ya saa 8:45 mchana jana Katika kijiji cha Olkungwando ,kitongoji cha Momela kata ya Ngarenanyuki ,Tarafa ya King’ori wilayani Arumeru.
Kamanda Moita amesema chanzo cha ajali hiyo ni upepo mkali,ambapo nahodha wa mtumbwi huo ni muongoza watalii katika kampuni ya Africa .
Aidha Kamanda Moita ametoa wito kwa watumiaji wa vyombo vya majini kuwa na tahadhari pindi kunapotokea mabadiliko ya hali ya hewa,na wawe na vifaa vyote vya uokoaji wawapo majini ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza.
Akitolea ufafanuzi wa kimbunga kilichotokea siku ya jana tarehe 1/10/2019 mkoani Arusha,majira ya saa 14:00 amesema kiliambatana na upepo mkali ambao uliweza kuezua vitu mbalimbali zikiwemo nyumba za ibada ,maduka pamoja na nyumba za watu binafsi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...