Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Chimuli, Kata ya Makole,mkoani Dodoma, John Fundi akimshukuru Naibu Katibu MkuuWizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima(aliyekaa katikati), kwa kujitokeza na kujiandikisha katikadaftari la wapiga kura. Kulia ni muandikishaji, Peter Ititi.


Na Mwandishi Wetu, MOHA

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Ramadhan Kailima, ametoa wito kwa watumishi wa umma na
Watanzania kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili
kutumia fursa hiyo kuchague viongozi wenye sifa karika
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Kailima aliyasema hayo Mjini Dodoma jana asubuhi baada ya
kujiandikisha katika daftari hilo kwenye kituo kilichopo Mtaa
wa Chimuli, Kata ya Makole.

Alisema uzoefu unaonyesha kuwa, kuna mwamko mdogo kwa
kundi la watumishi wa umma kujiandikisha, kushiriki uchaguzi
huo ili waweze kuchagua viongozi wenye sifa.

“Uchaguzi wa Serikali za Mitaa una umuhimu mkubwa kwa
maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla, uandikishaji huu
umeanza Oktoba 8-14, mwaka huu.

“Kampeni zitafanyika kwa wiki moja kuanzia Novemba 17-23,
mwaka huu, uchaguzi utafanyika Novemba 24, mwaka huu…ni muhimu jamii kutambua kuwa, mshindi katika uchaguzi huu atapatikana kwa idadi ya wapiga kura sio asilimia,” alisema.

Kailima alisema ni muhimu Watanzania wakashiriki uchaguzi
huo uli watumie fursa hiyo kuchagua kiongozi anayestahili,
wasiposhiriki atachaguliwa Mwenyekiti wa Serikali ama
mjumbe ambaye jamii kubwa haitapenda achaguliwe.

“Nawaomba wananchi wahudhurie kampeni, waulize maswali
kwa wagombea, watumie fursa hiyo kuchagua viongozi ambao
ni waadilifu na waaminifu.

“Rushwa ni adui wa maendeleo, wananchi mjiepushe kupokea
rushwa, Wizara yangu kupitia taasisi zake za ulinzi na usalama
ziko imara, tutaimarisha ulinzi wakati wa kampeni, upigaji kura
na utangazaji matokeo,” alifafanua.

Aliwapongeza waandikishaji, wasimamizi wa zoezi hilo kwa
kufika mapema kwenye vituo vya uandikishaji wapiga kura.
Alisema vituo hivyo viko sehemu barabarani, mitaani ambapo
uandikishaji huo hauna vikwazo kwani hauhitaji kitambulisho
cha uraia, cheti cha kuzaliwa.

“Ukifika kituoni utaulizwa majina yako kamili, umri wako, eneo
unaloishi…kama eneo lako la kujiandikisha sio hilo utaelekezwa
eneo la kwenda kujiandikisha,” aliongeza.

Kwa upande wao, mwandikishaji wapiga kura katika kituo
hicho, Peter Ititi na mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo, John

Fundi walimshukuru Kailima kwa wito alioutoa ili jamii ione
umuhimu wa kushiriki uchaguzi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...