Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amewahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao wenye umri chini ya miaka mitano kwenye Vituo vya Afya kupata chanjo bure hidi ya magonjwa ya Surua, Rubella na Polio kuanzia tarehe 17-21 Oktoba 2019.

Kwa Mkoa Mwanza, zaidi ya watoto laki sita (watoto 637,579) wanatarajiwa kupewa chanjo ya Rubella na Polio huku watakaopewa chanjo ya Surua wakitarajiwa kuwa zaidi ya elfu sitini (watoto 266,140) hivyo kufanya jumla ya watoto wanaotarajiwa kuchanjwa kuwa laki tisa elfu tatu  mia saba kumi na tisa (watoto 903,719). Kitaifa uzinduzi wa zoezi hilo umefanyika mkoani Morogoro, Oktoba 17, 2019.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye uzinduzi wa zoezi la utoaji chanjo dhidi ya Surua, Rubella na Polio.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akitoa salamu za Wizara kwenye uzinduzi wa zoezi la utoaji chanjo mkoani Mwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...