Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza na baadhi ya Watanzania waoishi nchini Korea, wakati alipokutana nao kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini humo na kuzungumza nao masuala mbalimbali yanayohusu Benki hiyo. Uongizi wa Benki ya CRDB ulifika ubalozini hapo kwa mualiko wa Balozi Matilda Masuka (kushoto), kwa nia ya kuipongeza Benki hiyo kwa kuwa Benki ya kwanza Afrika Mashariki na Kati, Kupokea kibali cha Umoja wa Mataifa cha Mfuko wa Hali ya Hewa ya Kijani (Green Climate Fund - GCF) itakayoweza kupitisha fedha za utekelezaji wa ufadhili wa kijani nchini Tanzania. Benki ya CRDB ilipata kibali hicho hivi karibuni wakati wa Mkutano wa 24 wa Bodi ya Hali ya Hewa ya Kijani (GCF), huko Songdo, Korea Kusini. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akipeana mkono na Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Balozi Matilda Masuka, baada ya hotuba yake kwa Umoja wa Watanzania waoishi nchini Korea.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay akizungumza katika Mkutano huo.

Baadhi ya Watanzania wanaoishi nchini Korea wakiwa kwenye Mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...