*WANATAALUMA WAJADILI MIKAKATI YA KUFIKIA UCHUMI WA KATI WA VIWANDA
Na Chalila Kibuda, Michuzi Tv
Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kimefanya  kumbukizi ya aliyekuwa Mkuu wa chuo  hicho  Marehemu Profesa  Joshua Doriye katika kutengamanisha  utumishi wake pamoja taaluma  ya utumishi wake uliotukuka .
Kumbukizi ya Profesa   Doriye  kitaaluma kwa wanafamilia ya IFM katika kuenzi na kufuata utumishi wake katika kufanya kazi sehemu mbalimbali kutokana na umahiri wake katika taaluma.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo cha  Usimamizi wa Fedha Profesa Tadeo Satta amesema kuwa katika kuangalia kumbukizi ya Profesa Doriye  ni pamoja na kuangalia taaluma katika kwenda katika uchumi wa viwanda  kwa kufungua fursa ya wanafunzi wanaohitimu kuingia katika uanzishaji wa viwanda.
Profesa Satta amesema serikali ya awamu ya Tano imechukua wataalam wengi ili kuweza kusaidia  na kushauri serikali kwenda katika mipango yake ya kuipeleka Tanzania kwenda katika uchumi wa kati wenye viwanda.
Amesema  kuwa wanafunzi wanaohitimu  kwa sasa ndio wanaweza kufikisha mipango ya serikali ya uchumi wa viwanda kwa kwenda na mawazo yao katika kufungua viwanda na kuzalisha ajira zingine ambapo serikali itakuwa imepiga hatua ya maendeleo inayoitaka.
Profesa Satta amesema kuwa kama wataalam wanaangalia pamoja na kushirikiana na nchi ambazo zimepiga hatua za kimaendeleo ikwemo India  ambayo imepiga hatua  kutokana na sera walizozianzisha zikazaa maendeleo.
Aidha amesema serikali imekuwa na mikakati mbalimbali ikiwemo na ya kisera katika kuandaa wataalam kuwa wazalishaji wa fursa za ajira kwa kuanzisha viwanda ambavyo vitazalisha ajira kwa watu wengine.

Katika Kumbukizi ya Marehemu Profesa Doriye mwenyekiti aliyeongoza  majadiliano ni Profesa Samuel Wangwe wa Daima Associate Limited  na mwasilishaji mada Profesa Arunaditya  Sahay  wa Taasisi ya Usimamizi wa Teknolojia ya Bibla nchini India.
 Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Profesa Tadeo Satta akizungumza na waandishi habari katika kumbukizi ya aliyekuwa Mkuu wa chuo hicho Marrehemu Profesa Joshua Doriye iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 mwasilishaji mada  wa Taasisi ya Usimamizi wa Teknolojia ya Bibla nchini India Profesa Arunaditya  Sahay akitoa mada katika kumbukizi ya aliyekuwa Mkuu wa chuo hicho Marrehemu Profesa Joshua Doriye iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti majadiliano ni wa Daima Associate Limited  Profesa Samuel Wangwe akiendesha majadiliano katika mada katika kumbukizi ya aliyekuwa Mkuu wa chuo hicho Marrehemu Profesa Joshua Doriye iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi na IFM na wataalam wakiwa katika mada katika kumbukizi ya aliyekuwa Mkuu wa chuo hicho Marrehemu Profesa Joshua Doriye iliyofanyika jijini Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...