Halmashauri ya Tandahimba imepokea wakimbizi 165 ambao wameingia Wilayani humo kwa madai ya kukimbia machafuko yanayoendelea nchini kwao.
Akizungumza Jana Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Said Msomoka alieleza kuwa wakimbizi hao wameingia kwa kupitia Mto Ruvuma hivyo halmashauri imewahifadhi katika Kijiji Cha Lipalwe B
"Tumewatoa kule bondeni tumewaleta hapa kijijini na tumewaandalia sehemu kwa ajili ya malazi na vile vile tumewaletea chakula ," alisema Msomoka
Naye Mkaguzi Msazidizi wa Uhamiaji Raymond Mapunda alieleza kuwa Kati ya idadi hiyo wanaume 37,wanawake 47,watoto wa kiume 33 ,watoto wa kike 28 na hivyo kufikia idadi ya 143 ,22 ni idadi ya raia wa Tanzania ambao nao walikuwa wakiishi huko
"Kabla ya kuwapokea wanakaguliwa ili kujiridhisha ili kuepuka kuwapokea wengine ambao huenda wakawa waharifu,lakini hata hivyo wanachi wafuate utaratibu wanapotaka kwenda nchi hiyo jirani kwa kufika katika ofisi za Uhamiaji Wilaya,"alisema Mapunda
Wakimbizi raia wa Msumbiji
Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji Wilaya ya Tandahimba Raymond Mapunda
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tandahimba Said Msomoka
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...